Print this page

Jimbo Segerea kutengenezwa

Na Mwandishi wetu

Mbunge wa Jimbo la Segerea Wilayani Ilala, Jijini Dar es Salaam, Bonnah Kamoli, amesema kuwa dhamira yake ni kuhakikisha barabara za Jimbo hilo zinapitika wakati wote, ikiwa ni pamoja na kujengwa kwa kiwango cha lami, zege au changarawe.
Kamoli alisema hayo katika hafla ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (Tanzania Rural and Urban Roads Agency: TARURA) Wilaya ya Ilala, kukabidhi mradi wa ujenzi wa barabara ya Zimbili-Kichangani ya kilomita 0.5 kwa Mkandarasi Kampuni ya SERC Constructions Co.Ltd, katika Kata ya Kinyerezi.

Rate this item
(0 votes)
Japhet