GEITA
Na Mwandishi wetu
Mbunge wa Jimbo la Busanda Tumaini Magesa ameahidi mwezi mmoja na nusu kukamilisha ujenzi wa bweni katika shule ya sekondari Lutozo iliyopo katika mamlaka ya mji mdogo wa Katoro mkoani Geita.
Ameyasema hayo aliposhiriki kuchimba msingi wa bweni hilo ambalo linatakiwa kutumika katika msimu mpya wa masoma ya Kidato cha Tano mwaka huu.