VATICAN CITY, Vatican
Baba Mtakatifu Fransisko anatarajiwa kufanya ziara yake ya kichungaji kwenye mji wa Maji katika Kisiwa cha Giudecca, Aprili 28 mwaka huu.
Katika ziara hiyo baba Mtakatifu atakuwa na hotuba tatu na mahubiri wakati wa takriban saa sita katika jiji la maji.
Aidha, atatembelea kituo cha wafungwa cha wanawake na kuwasalimia wasanii wa Biennale.
Aidha, Ataadhimisha Misa katika uwanja wa Mtakatifu Marko kabla ya kuingia kwenye Basilika na kuheshimu masalia ya Mtakatifu mlinzi, Patriaki Moraglia, Shukrani kwa Baba Mtakatifu kwa sababu alitaka kuweka makini Veneto na Kaskazini-Mashariki,kuanzia mji wetu.
Mkutano gerezani na wafungwa na kwa ajili ya uzinduzi wa banda la Vatican lenye kauli mbiu ya Afya; hatimaye kupita chini ya daraja na pantoni kwenda katika Uwanja wa Mtakatifu Marko kwa ajili ya Misa kuu, ikifuatiwa na sala ya kibinafsi kwenye kaburi la Mtakatifu Marko Mwinjili, mtakatifu msimamizi wa Venezia na watu wa Venezia.
Hizi ni nyakati tatu zitakazoadhimisha takriban saa sita za ziara ya kitume ya Baba Mtakatifu Fransisko huko Venezia, inayotarajiwa kufanyika inayoongozwa na kauli mbiu: “Kukaa na umoja katika upendo wa Kristo” na inayohamasishwa na ukurasa wa Kiinjili kuhusu tawi na mzabibu.
Mpango huo rasmi umechapishwa tarehe 25 Machi 2024 na Ofisi ya Vyombo vya Habari vya Vatican na kuwasilishwa katika Chumba cha Tintoretto cha Kasri na Patriaki wa Upatriaki wa Venezia, Kardinali Francesco Moraglia ambaye alisema kuwa katika siku ile ni ya mfano ambao unachukuliwa kuwa “siku ya kuzaliwa ya Venezia”, ambayo kwa kawaida inaaminika kuwa ilianzishwa mnamo mwaka 421.
Baba Mtakatifu Fransisko ataondoka saa 12.30 alfajiri kwa helikopta ya Vatican na kutua karibu saa 2.00 kamili asubuhi katika uwanja wa ndani wa Nyumba ya Gereza la Wanawake huko Venezia, kwenye Kisiwa cha Giudecca, ambapo atakaribishwa na Patriaki Francesco Moraglia, msimamizi Maria Milano Franco D’Aragona, Mkurugenzi Mariagrazia Felicita Bregoli, na kamanda wa Polisi wa Magereza, Lara Boco.