Print this page

Askofu Msipu ataka usawa katika ugawaji chakula

CHIPATA, Zambia
Askofu Msaidizi wa Jimbo Katoliki la Chipata Gabriel Msipu, ametoa wito wa ugawaji sawa wa chakula cha msaada wakati Serikali ikikabiliana na uhaba wa chakula unaotarajiwa kutokana na ukame, na kusisitiza kwamba hatua zinapaswa kuchukuliwa ili kuzuia vifo vinavyotokana na njaa.
Akiwa katika ziara ya kichungaji katika Parokia ya Mtakatifu Atanazio, Askofu Msipu alisisitiza umuhimu wa ugawaji sawa wa vifurushi vya chakula, akiahidi ushirikiano kati ya Kanisa, Mashirika Yasiyo ya Kiserikali, na Serikali kuhakikisha hakuna anayeachwa na njaa.

Rate this item
(0 votes)
Japhet