Print this page

Papa awasaidia waathiriwa wa mabomu

Magari yakiwa yamebeba mizigo ya misaada mbalimbali kuelekea nchini Ukraine. Magari yakiwa yamebeba mizigo ya misaada mbalimbali kuelekea nchini Ukraine.

VATICAN CITY, Vatican

Baba Mtakatifu Leo XIV ametuma misaada ya kifedha kwa ajili ya Dominika ya Familia Takatifu ili kusaidia familia zilizoathiriwa zaidi na mabomu ya Nchi ya Ukraine, ambapo umeme, maji na joto havipo.
Mwadhama Konrad Kardinali Krajewski, Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Upendo aliripoti “ubembelezaji mdogo” wa Papa Leo XIV, ambao umesababisha kutoa misaada ya kifedha kutumwa sehemu mbalimbali za dunia kusaidia familia hizo, ambapo Malori matatu ya misaada ya kibinadamu yaliwasili katika maeneo hayo yaliyoathiriwa.

Rate this item
(0 votes)
Japhet