DAR ES SALAAM
Na Mwandishi wetu
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi, amewataka walezi kuwapuuza vijana wanaojiita Wakatoliki, na kulipinga Kanisa Katoliki kuwa ni ‘fake’, na Ukristo wao hauna mizizi.
Askofu Mkuu Ruwa’ichi alitoa wito huo hivi karibuni wakati akitoa homilia yake, katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Shukrani ya Walezi wa Shirika la Kipapa la Utoto Mtakatifu Jimbo, iliyofanyika katika Parokia ya Mtakatifu Gaspar –Mbezi Beach.