MOSHI
Na Mwandishi wetu
Mkuu wa Jeshi la Polisi (Inspector General of Police: IGP) nchini, Camillus Wambura amesema kwamba takwimu za makosa makubwa ya jinai nchini yameongezeka katika kipindi cha Januari hadi Juni mwaka 2022.
IGP Wambura aliyasema hayo wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha maofisa wa waandamizi wa Jeshi la Polisi Makao Makuu, na makamanda wa Polisi wa Mikoa na Vikosi, akisema kuwa makosa hayo yameongezeka kutoka 24,848 kipindi kama hicho mwaka 2021 hadi makosa 27,848, sawa na ongezeko la asilimia 11.2.