Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha
Super User

Super User

Selfies labore, leggings cupidatat sunt taxidermy umami fanny pack typewriter hoodie art party voluptate. Listicle meditation paleo, drinking vinegar sint direct trade.

Jubilei hii ya Miaka 50 ya Wawata nchini, itafunguliwa na Misa Takatifu na kufuatiwa na Mashangilio ya Sherehe hii kubwa kwa WAWATA | Picha hizi zinatengenezwa na TUMAINI MEDIA. Matumizi yoyote ya picha hizi ni marufuku bila idhini kutoka TUMAINI MEDIA Hakimiliki © Tumaini Television - Haki zote zimehifadhiwa.Tafadhali Endelea Ku- Subscribe akaunti hii na bonyeza alama ya Kengele ili kupata taarifa zetu kwa wakati sahihi.

Na Arone Mpanduka

Chimbuko la bendi ya Maquis du Zaire kwa nchi ya Tanzania lilianzia mwaka 1973, wakati Franco Luambo Luanzo Makiadi akiwa na bendi yake ya T.P. OK. Jazz alikuja hapa nchini na akafanya onyesho kamambe katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam(sasa uwanja wa Uhuru).
Mwaka mmoja baadae wa 1972, bendi ya Maquis du Zaire, nayo ikaingia kwa mbwembwe na kuweka makazi yake ya kudumu katika jiji la Dar es Salaam.
Bendi hiyo Maquis du Zaire iliyotokea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ikafia humu nchini miaka ya 1990.
Ilikuwa kivutio kikubwa kwa Watanzania na kuwapa hekaheka wanamuziki wa Tanzania katika miaka hiyo.
Kwa nchini Congo, bendi hiyo ilianza mwaka 1960, vijana wa wakati huo katika mji wa Kamina huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), waliungana na kuunda bendi yao, wakaiita Super Theo.
Bendi hiyo ilikuwa ikitoa burudani tosha kwa wapenzi wa muziki wa mji huo wa Kamina na vitongoji vinavyouzunguka mji huo. Baadae wakaibadilisha majina na bendi ikawa Super Gabby. Lakini uongozi wa Super Gabby ulitaka kuleta mageuzi katika muziki mwaka 1972, walipobadilisha majina rasmi na kuwa Maquis du Zaire.
Mwaka huo huo bendi hiyo iliingia hapa Tanzania wakipitia nchini Uganda.
Walipofika katika jiji la Dar es Salaam, walipata mkataba wa kupiga muziki katika ukumbi wa Mikumi Tours, uliokuwa maeneo la Tazara Buguruni, jijini Dar es Salaam.
Baada ya kumaliza mkataba wao, waliondoka wakaenda kupiga muziki katika Klabu ya Hunters kwa kipindi kifupi.
Kisha viongozi wa bendi hiyo wakafanya mazungumzo na mfanyabiashara Hugo Kisima, aliyekuwa akimiliki ukumbi wa Safari Resort, maeneo ya Kimara, jijini Dar es Salaam. Wakaanza kupiga muziki kwa mkataba na mfanyabiashara huyo.
Februari 1977 viongozi wa bendi hiyo ya Maquis du Zaire, waliamua kukiongezea nguvu kikosi chao. Hivyo walimtuma Tchibangu Katayi ‘Mzee Paul’ aliyekuwa mwanamuziki wa bendi ya Maquis du Zaire.
Pia alikuwa mmoja kati ya viongozi wa bendi hiyo.Mzee Paul aliwachukua baadhi ya wanamuziki ili kuja nao Tanzania kuongeza nguvu katika bendi ya Maquis du Zaire.
‘Mzee Paul’ alibahatika kuwachukua wanamuziki akina Kikumbi Mwanza Mpango, au ‘King Kiki’, mtunzi na mwimbaji, Kanku Kelly kwa upande wa tarumbeta., Ilunga Banza ‘Mchafu’, aliyekuwa akiungurumisha gitaa la besi, Mutombo Sozy aliyekuwa akizicharanga ‘drums’, na mnenguaji Ngalula Tshiandanda.
Wakati huo Maquis du Zaire walikuwa wakicheza muziki wakitumia mtindo wa ‘Chakula Kapombe’, ambao kwa Watanzania ulikuwa mpya, na ukapendwa mno na mashabiki.
Kufika kwa wanamuziki hao, kulileta changamoto kubwa katika muziki. Tungo nzuri za Kikumbi Mwanza Mpango ‘King Kiki’, zilikuwa chachu masikioni mwa wapenzi wa muziki wa dansi. Kiki pia yaelezwa kuwa ndiye aliyeleta Mapinduzi makubwa ya muziki hapa nchini Tanzania.
Maquis du Zaire wakaazisha mtindo mwingine wa ‘Kamanyola’, uliowapagaisha wapenzi na wadau toka pembe zote za jiji la Dar es Salaam.
Mwishoni mwa 1977, Marquis du Zaire walimaliza mkataba kwa Hugo Kisima, wakaondoka.Bahati nyingine ikawadondokea tena baada ya kuingia mkataba mwingine wa kupiga muziki kwa mzee Makao, aliyekuwa akimiliki ukumbi wa Savannah, maeneo ya Ubungo.Wakiwa Savannah, walianzisha mitindo ya ‘Sanifu’, na ‘Ogelea piga mbizi’.
Lakini ukumbi huo ukabadilishwa jina ukaitwa White House. Ikumbukwe kwamba Maquis pia ilikuwa ikipiga kwenye ukumbi wa Mpakani, maeneo ya Mwenge.Mwishoni mwa mwaka 1978, Maquis du Zaire  waliamua kuimarisha tena kikosi chao kwa kuwaleta wanamuziki wengine wapya kutoka DRC.Iliwaleta akina Kabeya Badu, Kalala Mbwebwe, Ngoyi Mubenga na Khatibu Iteyi Iteyi.
Bendi hiyo ilikuwa ikiongozwa na wanahisa akina Chinyama Chiyaza ‘Chichi’, Chibangu Katayi ‘Mzee Paul’, Chimbwiza Mbangu Nguza au ‘Nguza Vicking’, Mutombo Lufungula ‘Audax’ na Mbuya Makonga ‘Adios’.
Chini ya uongozi huo, katika miaka ya 1980 mafanikio makubwa yalionekana, mojawapo ni lile la kuanzisha Kampuni iliyofahamika kama Orchestra Maquis Company (OMACO).
Kampuni hiyo iliweza kumiliki shamba la matunda, wakalima kwa kutumia trekta zao maeneo ya Mbezi nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam. Mazao yao walikuwa wakiyapeleka na kuuza katika Soko Kuu la Kariakoo jijini Dar es Salaam.OMACO pia ilimiliki mradi mwingine wa viwanja tisa na nyumba kadhaa, maeneo ya Sinza, jijini Dar es Salaam.
Kwa wakati huo, watu wengi hawakuwa na haja ya kuchukua teksi kurudi nyumbani, kwani muziki wa Maquis du Zaire ulikuwa unarindima hadi alfajiri. Muda ambao mabasi ya UDA ya Ikarus yalikuwa yameanza kazi. Wakati huo hazikuwepo ‘Dala dala’, Bajaji wala Pikipiki kwa maana ya Bodaboda.
Hata hivyo, baadae bendi hiyo ilianza kufa taratibu kufuatia baadhi ya wanamuziki kuondoka kwenda kutafuta maisha sehemu nyingine, na wengine kusahindwa kufanya kazi hiyo kutokana na umri kuwa mkubwa, na magonjwa ya hapa na pale.
Mwanzoni mwa miaka ya 1990, bendi ilipotea kabisa na kuacha historia ya kipekee.
Baadhi ya nyimbo za Marquis du Zaire zilizovuma kwa uzuri na utamu wake ni ‘Ni Wewe Pekee; Makumbele; Kalubandika; na Promotion’.
This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.

WAWATA watikisa Visiga

September 02, 2022

KIBAHA

Na Mathayo Kijazi

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Jude Thaddaeus Ruwa’ichi amewataka Wanawake Wakatoliki Tanzania (WAWATA), na waamini wote kutambua kwamba wanapomsifu Mtakatifu Agustino, wanapaswa pia kumshukuru Mama yake mzazi Mtakatifu Monica.
Askofu Ruwa’ichi aliyasema hayo wakati akitoa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Kilele cha Jubilei ya Miaka 50 ya Wanawake Wakatoliki Tanzania (WAWATA) Kijimbo, katika Kumbukumbu ya Mtakatifu Monica, iliyofanyika katika Seminari Ndogo ya Mtakatifu Maria, Visiga, jimboni humo.
“Tunaadhimisha mambo kadhaa, kwanza kabisa tunawamkumbuka WAWATA, na hususan Mtakatifu Monica, mama yake Mtakatifu Agustino. Huyu ni mama wa mfano, mama aliyetukuka, mama wa kuigwa. Mama huyu alizaliwa mwaka 331 katika Bara la Afrika, huko Afrika ya Kaskazini,” alisema Askofu Mkuu, na kuongeza,
“Alizaliwa na kulelewa vizuri katika familia ya Kikristo, akajenga na kustawisha fadhila zilizo njema; fadhila ya Imani; fadhila ya mapendo; fadhila ya huruma na fadhila za kimama. Tumtukuze Mungu kwa zawadi ya Mama huyu kutoka Bara la Afrika,” alisema Askofu Mkuu Ruwa’ichi.
Askofu Ruwa’ichi aliwapongeza WAWATA kwa kuendelea kusimama imara na kwa kujitolea kwao katika shughuli mbalimbali za Kanisa, huku akiwasihi kufahamu kwamba wao ni zawadi ya Mungu kwa Kanisa na Ulimwengu.
Askofu Mkuu Ruwa’ichi alimshukuru Mungu kwa utume unaofanywa na akinamama hao, hasa kuwalea Vijana wa Seminari ya Visiga, akimwomba Mungu awazidishie neema na baraka zake, ili utume wao uendelee kustawi, na kuutukuza ukuu wa Mungu.
Askofu Ruwa’ichi aliwasihi WAWATA kutafakari kwamba wao ni baraka kutoka kwa Mungu, kwa uwepo wao wa Miaka 50 sasa, kwani Utume wa Wanaume Wakatoliki (UWAKA), hata miaka 30 bado hawajafikisha, huku akiwasihi akinamama hao kumshukuru Mungu kwa mema yote anayowajalia.
Aidha, aliwaasa WAWATA kuendelea kubaki kuwa Wakristo Wakatoliki wazuri, hata katika Kanisa la nyumbani, kwa kusimama imara na kuwa mama bora, hata katika familia zao.
Kwa upande wao, Maaskofu Wasaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu na Mhashamu Stephano Musomba, waliwapongeza WAWATA kwa kuadhimisha Jubilei yao ya Miaka 50, na kwa kazi nzuri ya utume wanaoendelea nao kuufanya jimboni humo.
Naye, Mwenyekiti wa Wanawake Wakatoliki Tanzania (WAWATA), Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Stella Rwegasira aliwashukuru waamini wote walioshiriki Adhimisho hilo.
Aidha, Catherine Mwingira, Katibu wa WAWATA Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam alisema kuwa wanamshukuru Mungu kwa kufikisha Miaka 50 tangu chama hicho cha Kitume kuanzishwe na waasisi wao, huku akisema kuwa yamefanyika mengi mazuri tangu kuanzishwa kwa chama hicho hadi sasa.
Chama cha Kitume cha Wanawake Wakatoliki Tanzania (WAWATA), kilianzishwa rasmi mwaka 1972.

MOROGORO

Na Angela Kibwana

Mhashamu Askofu Lazarus Msimbe -SDS, wa Jimbo Katoliki la Morogoro, ametoa wito kwa Mapadri kutohubiri Injili ya mafanikio, kwa sababu kuna desturi ambayo inataka kuzuka hata ndani ya Kanisa Katoliki, kwa sababu baadhi ya waamini kutaka miujiza na mafanikio, hali inayosababisha baadhi yao kuhamia Makanisa mengine.
Askofu Msimbe alisema hayo katika mahubiri wakati wa kutoa Daraja la Upadre kwa Mashemasi wanne wa Shirika la Wasalvatorian, iliyofanyika Chuo Kikuu Kishiriki cha Jordan, Jimboni Morogoro.
Aidha, Askofu Msimbe alisema kuwa Mapadri wanapaswa kuhubiri Injili ya Yesu, ambayo si Injili ya kutaka mafanikio. Hivyo, ni kazi ya Mapadri kuwaeleza waamini ukweli, kwamba hakuna mafanikio yanayoweza kujitokeza bila kuvuja jasho, au kufanya kazi kwa bidii.
 Alisema kuwa kutokana na desturi iliyozuka kwa waamini wengi kutekwa na injili ya miujiza na mafanikio, Askofu Msimbe ametumia nafasi hiyo kuwatahadharisha Mapadre kutojihusisha na mitego ya kudanganya watu kukanyaga waamini wao, kukanyaga mafuta ya upako, kwa kigezo cha kujipatia utajiri.
Alibainisha kuwa Mapadri wanatakiwa kuwahubiria watu ukweli kwamba kuna mateso katika safari ya kutafuta mafanikio, waamini wanahitaji kufundishwa mbinu bora za kuwa na mipangilio mizuri, kwa sababu hakuna mtu anayeweza kupata mafanikio kwa njia rahisi.
Hata hivyo aliwaonya Mapadri, kutozigeuza Baraka zao kuwa biashara kwa sababu wamepewa bure ili kuwahudumia watu. Wasiuze baraka zao, jambo la msingi kwao ni kuhakikisha wanahubiri injili ya Yesu ambayo haitaki ulaini katika maisha.
Mapadri wanapaswa kutambua kuwa wao ni mbegu ambayo inapaswa kumea vizuri kwa kufanya mambo yampendezayo Mungu, kwani ni kielelezo katika kuyaenzi matakatifu, kwa kuwa kazi moja na muhimu ya mapadri ni kuhubiri Neno la Mungu, na wala siyo kujisifia wenyewe.
Alisema kuwa maadhimisho ya Sakramenti mbalimbali za Kanisa ndiyo dira inayoweza kumtambulisha Padre. Mapadre waepuke tabia ya kujisifia wenyewe, hivyo watu watatambua uzuri wa Padre kulingana na huduma makini kwa watu wake, hasa uadhimishaji wa Misa Takatifu.
Katika kuadhimisha Masakramenti, hasa Sakramenti ya Kitubio, Mapadri wanapaswa kuwa makini kuwatia moyo waamini wanapofanya kitubio ili kuwapatanisha na Mungu, na wala waamini wasikatishwe tamaa.
Sambamba na hayo, amewaomba mapadre hao wapya kushiriki maisha ya Jumuiya na kuziishi karama za Shirika la Wasalvatoariani, waishi kadri ya nadhiri zao kwa kuzingatia mambo ya msingi yanayowatambulisha kuwa WATAWA.
Wanapaswa kuzingatia maisha ya sala ambayo yatawasaidia kutimiza mapenzi ya Mungu na kufanya utume watakaopangiwa na wakubwa wao wa shirika, ili watekeleze kwa uaminifu na kwa uangalifu.
Aliwaomba waamini na watu wenye mapenzi mema kuwaombea Mapadri wapya na wengine waliotangulia katika utumishi huo kuwa wafuasi wema wa Kristo, ili kuwavuta vijana wengi wanaotamani kujiunga na wito huo Mtakatifu.
Mapadre wapya ni Padri Edward Lupaka, Padri Deogatius Silayo, Padri Erasmus Kayongo, na Padri Musa Ndelule.

KAYANGA

Na Angela Kibwana

Jimbo Katoliki la Kayanga ni mojawapo kati ya Majimbo 34 ya Kanisa Katoliki nchini Tanzania, ambalo limo katika Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza.
Jimbo hili linaundwa na wilaya mbili ambazo ni wilaya za Karagwe na Cherwa. Upande wa kaskazini linapakana na Uganda-Jimbo Kuu Katoliki la Mbarara. Upande wa Magharibi linapakana na Rwanda, na upande wa Mashariki linapakana na Wilaya ya Misenyi na kusini linapakana na wilaya ya Ngara nchini Tanzania.
Jimbo Katoliki la Kayanga lilitangazwa rasmi na Baba Mtakatifu Mstaafu Benedict XVI Agosti 14 mwaka 2008, ambalo lilimegwa kutoka Jimbo Katoliki la Rulenge – Ngara, na hatimaye kuzaliwa majimbo mapya mawili, yaani Jimbo Katoliki la Rulenge – Ngara, na Jimbo Katoliki la Kayanga.
Kunako mwaka 1929 ilianzishwa  Apostolic Vicariate ya Rulenge-Ngara kutokana na Apostolic Vicariate ya Tabora, ambapo Machi 25  mwaka 1953 Rulenge ilitangazwa kuwa Dayosisi. Hivyo, tarehe 14 Agosti 2008, ikamegwa Dayosisi ya Rulenge na hivyo kuanzishwa Jimbo Katoliki jipya la Kayanga.
Jimbo Katoliki la Kayanga lilizinduliwa Novemba 06 mwaka 2008, ambapo Askofu Almachius Vincent Rweyongeza aliwekwa wakfu akiwa Askofu wa kwanza wa jimbo hilo lenye kilomita za mraba 70,716 likiwa na wakazi zaidi ya laki 6, Wakatoliki wakiwa ni asilimia 60 Jimboni humo, kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2012.
Jimbo Katoliki la Kayanga lilianzishwa likiwa na Mapadri 24, hivyo kwa wastani, kila Padri mmojawao anahudumia waamini 11,200 katika Parokia 11 ilivyokuwa katika mwaka wa 2008, idadi ya watawa wa kike walikuwa 61 wa Shirika la Kijimbo.
Katika muktadha huo, Mhashamu Askofu Almachius Rweyongeza wa Jimbo Katoliki la Kayanga anamshukuru Mungu kwa mafanikio ya kiroho yaliyopatikana Jimboni humo, hasa ongezeko la Mapadre, Watawa wa kike, na Makatekesta ambao wamekuwa chachu ya kuimarisha katekesi kwa waamini.
Anabainisha kuwa hadi sasa Jimbo hilo lina jumla ya Mapadre 51, Watawa 94 wa kike, na ongezeko la Makatekesta kutoka 398 katika kipindi cha mwaka 2008, na kufikisha idadi ya Makatekesta 438 kwa mwaka 2022.
Aidha, alisema kuwa kwa kipindi cha miaka 14 tangu kuanza kwa Jimbo hilo kunako mwaka 2008 hadi mwaka huu 2022, kumekuwa na ongezeko kubwa la wahudumu, hasa Mapadre na miito ya Upadre, ambapo kwa mwaka huu amewapatia Daraja Takatifu Mapadre wapya watatu, na kufikisha idadi ya Mapadre 51 jimboni humo.
Hata hivyo ametaja pia mafanikio mengine, hasa ongezeko la familia za Kikatoliki kupitia Sakramenti ya Ndoa Takatifu, hali iliyosaidia kupunguza ndoa za mseto, uchumba sugu, ndoa mgando, ndoa za mitala, pamoja na kupungua kwa ndoa za kiserikali.
Miongoni mwa mafanikio mengine jimboni humo ni ongezeko la Jumuiya Ndogo Ndogo za Kikristo kutoka Jumuiya 1,039 hadi kufikia Jumuiya 1657, pamoja na uwepo wa Vituo vya Hija ambavyo amevitaja kuwa ni ‘Zahanati za Kiroho’ kwa ajili ya kutibu mahangaiko ya waamini.
Alisema kuwa wakati jimbo linazinduliwa lilikuwa na Parokia 11 tu, Vigango 234, Jumuiya za Kikristu 1,039 na Mapadre 24, Masista wa Jimbo 61 wa Shirika la Mitume wa Upendo, Upendo ambalo ndilo Shirika la Jimbo Katoliki la Kayanga, wakiwamo Makatekesta 398.
“Wahenga wetu wamesema ‘daima mwanzo ni mgumu’, ugumu huu ulitokana na shida za kiuchumi, hasa kuweka miundombinu ya msingi ya kichungaji na kijamii.
Namshukuru Mungu wakati jimbo linazinduliwa, Kanisa Kuu la Mtakatifu George, Kayanga, lilishajengwa na kutabarukiwa na Askofu Severine Niwemugizi wa Jimbo Katoliki la Rulenge - Ngara, Septemba 1, 2008, siku tano kabla ya kuzinduliwa kwa Jimbo Katoliki la Kayanga” alisema Askofu huyo.
Askofu Rweyongeza anasema kwamba alipokabidhiwa Jimbo la Kayanga hakuwa na uzoefu wowote wa kuzindua jimbo, hakuwa na ujanja wala mbinu za kuongoza jimbo hilo. Hivyo, aliandika katika Ngao yake ya Kiaskofu akijisalimisha kwa Bwana kwa kutumia maneno yasemayo: “Mimi ni Mtumishi wa Bwana.”
“Nilijisalimisha kwa Mungu kwa kutumia maneno ya Bikira Maria. Nilimkabidhi yote Mungu kwa sababu Mwenyezi Mungu asipojenga Jimbo Katoliki la Kayanga, wajengao wanajisumbua bure, nami nikiwa mmojawapo. Kusema kweli, Mwenyezi Mungu amenitendea makuu kwa kipindi cha miaka 14, kwani nimeshuhudia mafanikio makubwa,” alisema Askofu Rweyongeza.
Anasema vile vile kuwa licha ya idadi ndogo ya Mapadri wanaotoa huduma za kiroho Jimboni humo, anashukuru pia mchango wa Makatekesta ambao ni wasaidizi wa karibu wa Mapadre, hasa Vigangoni na Vijijini, kwa sababu Parokia moja inakuwa na vigango zaidi ya 30 ambavyo vinahudumiwa na Mapadre wawili, hivyo  Makatekesta wanasaidia sana kutoa huduma za kiroho kwa waamini wao.
Anasema kuwa hadi sasa kuna ongezeko la Parokia, kutoka 11 katika kipindi cha mwaka 2008, na sasa imefikia idadi ya Parokia 20 mwaka huu 2022, zenye Mapadre wenye makazi maalumu  katika Parokia hizo.
“Mapadri bado ni wachache kulingana na idadi ya Waamini Jimboni humu, kwani baadhi ya Parokia moja moja anaishi Padre mmoja tu, ambapo inakuwa ni kazi ngumu. Hata hivyo naamini kwamba Mungu ndiye anayeweza kutufanikishia kwa kuwategemeza katika Utume wa Kanisa licha ya uchache wao.”
Mbali na hayo, Askofu Rweyongeza amesifu ongezeko la Vyama vya Kitume Jimboni humo, ambavyo ni uhai wa Kanisa na Jimbo, na alivitaja kuwa ni Utoto Mtakatifu, WAWATA, UWAKA, VIWAWA, Lejio ya Maria, Wafransiskani na vyama vingine vya kitume, ambavyo ni chachu ya mafanikio ya kiroho Jimboni humo.
Amewasifu pia Viongozi wa Halmashauri Walei Katoliki (HAWAKA), ambao ni washiriki wenza katika shughuli za uchungaji ambao umejengwa na viongozi wanaojituma, ili kuhakikisha Jimbo linasonga mbele kiimani.
Sambamba na hayo kwa upande wa taasisi za Dini, ametaja uwepo wa Vituo vya Hija ambavyo ni ‘Zahanati za Kiroho’ zinazosaidia Waamini wengi Wakatoliki na wasio Wakatoliki kwenda kuchota neema na baraka kutoka katika vituo hivyo vya hija na maisha ya kiroho.
“Nilivizindua Vituo hivi vya hija  wakati Jimbo lilipoanza. Nikaona kwamba hili ni hitaji kubwa la kuwasaidia Waamini na jamii kuhusu masuala mbalimbali ya kiroho, kiimani na uponyaji, nikiamini kwamba Vituo hivi vya Hija ni zahanati za kiroho.”
Kalvario Kayungu ni miongoni mwa Vituo vya Hija jimboni humo, kilichozinduliwa septemba 14 mwaka 2011 kwa heshima ya Msalaba Mtakatifu. Pia, kituo kingine cha hija cha Lurd Bughene kilijengwa kwa heshima ya Bikira Maria wa Lurd  na Afya ya Wagonjwa, kikizinduliwa Februari 11, mwaka 2012.
Askofu Rweyongeza anasema kuwa familia ya Mungu Jimboni humo huwa wanafanya hija za kijimbo kila Februari 11, Kitaifa na Kimataifa huko Lurd Bughene katika kuadhimisha sikukuu ya Bikira Maria wa Lurd na Afya ya Wagonjwa. Pia, wanafanya hija za kijimbo, kitaifa na kimataifa huko Kalvario Kayungu kila ifikapo Septemba 14, kwa heshima ya kutukuka  kwa Msalaba.
Licha ya Jimbo hilo kuwa miongoni mwa majimbo machanga nchini Tanzania, limewekeza katika taasisi mbalimbali za jamii, hususan zinazogusia masuala ya Elimu kama vile shule, vituo vya afya hosptatali na zahanati, pamoja na tasisi za mazingira (CHEMA).
“Tuna taasisi muhimu sana Jimboni ijulikananyo kama CHEMA, kifupi cha Community Habitat Environment Management, kama mwitikio kwa Baba Mtakatifu kuhusu barua yake ya kitume ‘Laudato Si’ , inayohusika hasa na utunzanji wa mazingira,” alisema.
Anaeleza kwamba Taasisi ya CHEMA inashughulika na mazingira, kama vile upandaji miti na utengenezaji wa vitalu mbalimbali vya miti mbalimbali ya matunda na miti ya mbao, kivuli na biashara. Pia, ikiwemo utengenezaji wa majiko sanifu yanayotumia kuni kidogo, au majiko yanayotumia unga wa mbao kunusuru uangamizaji wa miti kwa ajili ya kujipatia kuni na mkaa, sanjari na ufugaji wa nyuki.
Wakati huo huo Askofu Rweyongeza anabainisha kwamba uharibifu wa mazingira ni moja kati ya changamoto zinazolikumba Jimbo hilo, hususani uharibifu wa vyanzo vya maji; ukataji wa miti kiholela; uchomaji moto misitu; na utumiaji wa sumu kuua magugu kwa kulima mazao ya muda.
“Jimbo langu limekumbwa na uharibifu wa mazingira, kwani mtu anakata mti wa miaka 30 ili apande mazao ya haraka kujipatia pesa ya haraka, bila kuangalia ni aina gani ya uharibifu wa mazingira anaousababisha.”
Kupitia taasisi ya CHEMA, Askofu Rweyongeza anasema kwamba anahimiza watu waoteshe miti ili kuhakikisha wanatunza uoto uliopo kwa sababu ya uharibifu wa mazingira, kwani ni hatari katika maisha ya binadamu na viumbe vyote.
“Jimbo Katoliki la Kayanga linao msitu wa mfano kuhakikisha kwamba mazingira yanatunzwa, nami namshukuru Mungu nina msitu wangu wa mfano ambao unaitwa bustani ya Edeni, ambako lengo ni kutunza miti ya asili ya matunda ambayo imeshatoweka. Nimepanda miti ya Kibiblia ambayo ni mizeituni, mitende, mitini na mizabibu, ambayo ninayo kwenye shamba langu la ekari 05”.
Itaendelea wiki ijayo.

DAR ES SALAAM

Na Philip Komba

Pamoja na mji wa Yerusalemu kujulikana zaidi sana kutokana na umaarufu wake katika mambo ya dini, mji huo haujabaki nyuma katika masuala ya muziki wa kidunia.
Kuna kikundi kimoja kikongwe cha muziki cha hapo mjini Yerusalemu, kiitwacho kwa lugha ya kigeni “The Jerusalem Symphony Orchestra” yaani Kikundi cha Muziki wa Simfoni cha mjini Yerusalemu. Kikundi hicho kimekuwa kikitamba sana katika fani hii ya muziki kuanzia miaka ya 1940.
Kutokana na umaarufu wake, kikundi cha muziki cha Simfoni cha Yerusalemu kimewahi kutembelea nchi mbalimbali za Kimagharibi na Kimashariki na kujizolea sifa nyingi.
Kikundi kingine kikubwa cha muziki kinajulikana kwa jina la “The Israel Philharmonic Orchestra” yaani kikundi cha Kiisraeli cha Wapendao muziki. Makao makuu ya kikundi hicho yamo katika lile jengo la Kituo cha Kimataifa cha Mapatano- “The International Convention Center” ambacho kiko karibu na lango kuu la kuingilia mjini Yerusalemu.
Shughuli zingine zinazowakilisha sanaa mjini Yerusalemu ni nyumba za sinema, kumbi za muziki kama ule ukumbi  mmoja maarufu ulio upande wa kusini mwa mji, na zingine tena mbili, moja ulio eneo la Yemin Mosha, na mwingine eneo la Ein Keren.
Vilevile kuna uwanja mkubwa wa matamasha ya muziki wa nje unaotumiwa pia na wasanii wa kimataifa kwa michezo ya kuigiza  na kwa nyimbo.
Michezo ya aina hii imekuwa ikifanyika kila mwaka tangu mwaka wa 1961 na Yerusalemu imekuwa ikiratibu michezo hiyo. Ukumbi mwingine wa shughuli za ukumbi wa michezo wa mjini Yerusalemu ni ule ulio karibu na Jalbiya.
Ukumbi huu unajulikana kwa kuwa na michezo ya kimataifa, ambayo inafikia zaidi ya michezo 150 kwa mwaka. Kuna kikundi kingine cha aina yake ambacho kinapendwa sana kutokana na utaratibu wake wa kubadilisha wachezaji mara kwa mara.  Makao makuu ya kikundi hicho yako karibu na kituo cha reli cha zamani cha hapo mjini Yerusalemu.
Maeneo mengine ya kuvutia mjini Yerusalemu: Bustani ya wanyama wa kibiblia: Bustani hiyo kimekuwa kivutio cha kwanza kwa watalii wote wanaoitembelea Israeli. Eneo jingine tena ni lile la Nyumba ya Ticho.
Nyumba hii iliyopo sehemu ya kuelekea chini ya mji wa Yerusalemu ina shughuli nyingi za kibiashara. Imepewa hilo jina la Ticho kwa sababu ina michoro na sanamu nyingi za Anna Ticho na za mume wake aliyekuwa mtaalamu wa kuchunguza macho.
Mtaalamu huyu ndiye aliyeanzisha kliniki ya kwanza ya macho katika jumba hilo hapo mwaka 1912. Jumba jingine mashuhuri mjini Yerusalemu ni lile la sanaa la Ah-Hoash lililoanzishwa mwaka 2004. Jumba hilo linatumika kwa kuhifadhia sanaa za Kipalestina.
Mwaka 1974 ilifunguliwa ofisi ya kuchunguza shughuli zote zinazohusiana na uonyeshaji wa sinema. Ofisi hii ilihamishiwa kwenye jengo jipya mwaka 1981 karibu na barabara ya Hebron kwenye bonde la Hinnom karibu na mji wa zamani.
Mji wa Yerusalemu ulitangazwa rasmi kama makao ya kitaifa ya ukumbi wa michezo ‘thieta’ ya Kipalestina inayojihusisha na shughuli za kuvumbua, kuhifadhi, na kuendeleza sanaa za Kipalestina. Makumbusho ya kitaifa ya muziki ya Edward Said ni mlezi wa kikundi cha muziki cha vijana wa Kipalestina.
Kikundi hicho cha vijana kimewahi kuzitembelea nchi za Kiarabu za Ghuba na nchi zingine kadhaa za Mashariki ya Kati hapo mwaka 2009. Jumba la Makumbusho la Kiislamu lililo kwenye Mlima wa Hekalu lilianzishwa mwaka 1923.
 Jumba hili linahifadhi vyombo vingi mbalimbali vya kale, kuanzia vile vidogo kabisa kama viriba vya wanja wa manga na miswada ambayo ni  adimu sana kupatikana siku hizi, hadi pandikizi za nguzo za marumaru.
 Pale Palestina inapokubali na kuidhinisha na hata kuziunga mkono za kifedha, baadhi ya shughuli za kitamaduni za Kiarabu, matukio muhimu ya Kiarabu yalipigwa marufuku kwa sababu yalifadhiliwa na Mamlaka ya Kitaifa ya Kipalestina.
Mwaka 2009, kulifanyika tamasha la kiutamaduni lililochukua siku nne na kuhudhuriwa na watu zaidi ya 15000 kule Beit ‘Aman pambizoni mwa mji wa Yerusalemu.’
Mfuko wa Fedha wa Abrahamu na Kituo cha Kimataifa cha Yerusalemu vinasaidia kwa kushirikiana kuendeleza miradi ya pamoja ya Kiutamaduni ya Kiyahudi na ya Kipalestina.
Kituo cha Yerusalemu cha Muziki wa Dansi wa mtindo wa Kimagharibi na wa Kimashariki, kinatoa warsha na semina za mawasiliano ya mazungumzo kwa njia ya sanaa.
Kikundi cha Muziki cha Muungano wa vijana wa Kiyahudi na wa Kiarabu kinapiga muziki wa dhati wa Kimashariki na wa Kimagharibi pia.
Mwaka 2006 ilifunguliwa njia ya burudani inayoyafikia maeneo mengi ya kiutamaduni, viwanja vya michezo na bustani za mapumziko ya starehe ndani ya eneo la mji wa Yerusalemu na maeneo mengine yanayouzunguka mji huo.
Mwaka 2008 ilisimikwa Sanamu ya Kuchongwa iliyotayarishwa na Czeslaw Dzwigaj juu ya mlima kati ya eneo la Wayahudi la Armon HaNetziv na lile la Kiarabu la Jebl Mukaber, kama dalili ya kiu inayosababishwa na hali ya kukosekana kwa amani.

Njia ya Mawasiliano:
Yerusalemu ni kituo cha Kitaifa cha kutawanya habari kwa njia ya radio na televisheni. Ofisi kuu ya Mamlaka ya Njia za Mawasiliano ya Israeli yako Yerusalemu pamoja na telivisheni na studio za radio ya Israeli idhaa Na. 2 na ya Na. 10 na sehemu ya studio za radio ya (British Broadcasting Corporation; BBC) taarifa ya habari.
Makao makuu ya magazeti ya “Jerusalem Post” na “The Times of Israel” la “KolHa’lr” na “The JerusalemTimes” na Kituo cha televisheni ya Kikristo kiitwacho “God Tv” yako pia Yerusalemu.
 
Uchumi:
 Kihistoria, uchumi wa mji wa Yerusalemu ulitegemea kabisa safari za hija za mahujaji waliokuwa wanafika kuhiji hapo Yerusalemu kwa  kuwa mji huo uko mbali na bandari za Jaffa na Gaza.
 Mambo yanayoipambanua Yerusalemu na kuwavutia wageni kutoka nchi mbalimbali ulimwenguni, siku hizi ni yale yanayohusiana na itikadi za dini, na pia mambo ya kiutamaduni wa Kiyahudi.
Wengi wa wageni hao wanafika kuuona ule ukuta wa upande wa magharibi na ule mji mkongwe. Mwaka 2010 Gazeti la “Travel plus Leasure magazine” liliutaja mji wa Yerusalemu kuwa ni mji ulioongoza kwa safari za wakati wa mapumziko katika Mashariki ya Kati na katika Bara la Afrika.
 Mwaka 2013, asilimia 75 ya watalii milioni 3.5 waliitembelea nchi ya Israeli na kuzuru mji wa Yerusalemu.
Tangu Serikali ya Israeli ilipoundwa, serikali ya kitaifa imebaki kama msimamizi mkuu wa uchumi wa mji wa Yerusalemu. Serikali iliyo mjini Yerusalemu, hutoa nafasi nyingi za kazi na hutoa pia ruzuku na marupurupu kwa wafasiria mali na kwa wale wanaoonekana kuinukia katika masuala ya kibiashara.
Ingawa mji wa Tel Aviv unabaki kitovu cha uchumi kwa upande wa fedha, idadi ya makampuni yenye teknolojia ya hali ya juu inazidi kuhamia Yerusalemu leo kila kukicha.
Makampuni hayo yalitoa nafasi za kazi 12000 mwaka 2006.
Maeneo yenye shughuli nyingi za viwanda na utafiti wa kiteknolojia, ni yale yaliyo upande wa kaskazini na upande wa kusini wa mji wa Yerusalemu.
Upande wa kaskazini, kwa mfano, kuna kiwanda cha ‘Har Hotzvian’ pamoja na eneo la utafiti wa masuala ya kiteknolojia na wa maendeleo ya viwanda.
Upande huo wa kusini mwa mji wa Yerusalemu kuna pia viwanda kama vile viwanda vya madawa vya Intel, Cisco, Teva; IBM, Mobileye and Johnson, Medironic na vingine vingi.
Mwezi Aprili, 2015, Gazeti la “Time Magazine” liliuchagua mji wa Yerusalemu, kama moja ya kitovu kinachojitokeza kati ya miji mitano ulimwenguni likiutamka mji huo kwa kusema kuwa mji wa Yerusalemu umekuwa kitovu  kinachojitahidi kuendeleza uuishaji wa vifaa mbalimbali, kama kwa mfano, vifaa vya kufanyia usafi, vifaa vya uchangamshaji na urahisishaji wa ufanyaji kazi wa inteneti n.k.                             
Kukua kwa mji wa Yerusalemu kiuchumi na uendelezaji wa uchumi huo:
Ingawa takwimu zinaonyesha kuwa mji wa Yerusalemu kwa ujumla wake umekuwa ukikua kiuchumi kuanzia mwaka wa 1967, hali ya mji wa Yerusalemu ya mashariki si nzuri sana ikilinganishwa na ile ya magharibi kwa hali ya uchumi wake.
Hata hivyo, familia za jumuiya za Kiarabu zina watu wengi zaidi walioajiriwa ambao wamefikia asilimia 76.1, zikilinganishwa na zile za Kiyahudi ambazo zina asilimia 66.8 tu.
Idadi ya wale wasioajiriwa katika mji wa Yerusalemu, ambao ni asilimia 8.3 ni afadhali kidogo ikilinganishwa na wastani wa wasioajiriwa kitaifa, ambao wanafikia wastani wa asilimia 9.0.
Umaskini unabaki bado ni tatizo katika mji wa Yerusalemu kwa kuwa asilimia 37 ya familia katika mji huo zilikuwa zinaishi chini ya mstari wa umaskini hapo mwaka 2011.
Kwa mujibu wa ripoti ya Shirikisho la Haki za Kijamii katika nchi ya Israeli, asilimia 78 ya Waarabu katika mji huo wa Yerusalemu walikuwa wakiishi kimaskini hapo mwaka 2012. Kiwango hicho kilikuwa kimeongezeka toka asilimia 64 mwaka 2006.
Shirikisho la Haki za Kijamii linadai kuwa, hali hii imesababishwa na kukosekana kwa ajira, muundo msingi na mfumo wa elimu usiokidhi. Ir Amin, mmoja wa viongozi wa Kiarabu, hata hivyo, anailaumu hali hii, akisema kuwa imesababishwa na ile hadhi ya kisheria waliyopewa Wapalestina katika mji wa Yerusalemu.
Ujenzi wa maghorofa katika mji wa Yerusalemu: Kijadi, mji wa Yerusalemu, umekuwa muda wote na majengo ya urefu wa kawaida tu.
Kulikuwa na majengo 18 tu katika mji wa Yerusalemu yaliyojengwa kwa wakati tofauti, ambayo yalikuwa na urefu wa kwenda juu zaidi ya ule wa kawaida.
Majengo haya yalikuwa yamejengwa kuelekea upande wa seheme ya chini ya mji, wakati ule ambao hakukuwa na sheria zilizokuwa wazi kuhusu ujenzi mijini. Jengo moja kati ya hayo majengo 18 ni lile liitwalo jengo la “Holy Land Tower No.1”.
Jengo hili lenye ghorofa 32, ndilo jengo refu kuliko majengo mengine yote mjini Yerusalemu. Jengo jingine la kufanana na hili ambalo nalo litaitwa “Holyland Tower”, lakini No. 2”  ujenzi wake umekwisha kuidhinishwa na mamlaka husika. Jengo hili nalo litakuwa na urefu uleule wa ghorofa 32.
Mpango Mkuu mpya wa mji wa Yerusalemu una majengo mengi marefu yakiwa pamoja na yale ambayo ni marefu sana yatakayojengwa katika baadhi ya maeneo fulani teule kuelekea sehemu ya chini ya mji wa Yerusalemu.
Kwa kuzingatia mpango huo, kutakuwa na mstari wa majengo kandokando ya barabara ya Jaffa na pia kandokando ya mtaa wa “King George”.
Jengo moja refu kati ya yale yaliyopendekezwa kujengwa kandokando ya barabara ya Jaffa na kandokando ya mtaa wa “King George” litakuwa na ghorofa 65 na litakuwa jengo refu kuliko majengo mengine yote nchini Israeli.
Kwenye lango la kuingilia mjini Yerusalemu, karibu na Daraja la ‘Chords’ na Kituo cha Kati cha Reli, kutajengwa maghorofa mengine yatakayokuwa na urefu wa kati ya ghorofa 24 na ghorofa 33.
Majengo haya yatakuwa sehemu ya eneo litakalokuwa na nafasi wazi kwa shughuli mbalimbali na pia kutakuwa na kituo cha reli ya chini kwa chini.
Kituo hicho cha reli kitaunganishwa kwa madaraja na pia kwa barabara za chini kwa chini. Kituo hicho cha reli nacho kitatoa huduma kwa treni za mwendo kasi kati ya Yerusalemu na mji wa Tel Aviv.
Majengo kumi na moja kati ya hayo maghorofa marefu yatatumika kama ofisi au nyumba za kupangisha na jengo moja litakuwa hoteli kubwa ambayo itakuwa na nafasi za kutosha kwa watu 2000.
Majengo haya yanategemewa kuwavutia wafanya biashara wengi kutoka mji wa Tel Aviv na hivyo kupafanya mahali hapo  kuwa kitovu muhimu cha shughuli za kibiashara.
Zaidi ya shughuli hizo za kibiashara, kutajengwa pia katika eneo hilo hilo kumbi na ofisi za mahakama pamoja na ofisi ya mwendesha mashtaka wa serikali.
Katika eneo hilo kutajengwa pia majengo ya makao mapya ya Hifadhi ya Nyaraka za Kiyahudi na majengo kwa ajili ya Hifadhi ya Nyaraka za Serikali ya Israeli.
Majengo marefu yote yaliyojengwa mjini Yerusalemu yanategemewa kuacha nafasi kwa wananchi ya kuwawezesha kujiburudisha, nafasi kwa ajili ya mikahawa na nafasi kwa ajili ya maduka. Utaratibu huu unaweza kuichangamsha sehemu hii ya mji wa Yerusalemu.
Mwezi wa Agosti mwaka wa 2015, halmashauri ya mji wa Yerusalemu iliidhinisha ujenzi wa jengo refu la futi 344, lenye umbo la kipiramidi.
Mchoro wa jengo hilo ulitayarishwa na Daniel Libeskind kwa kushirikiana na Yigal Levi badala ya mchoro uliokuwa umeandaliwa hapo awali. Jengo hilo lilianza kujengwa mwaka 2019.

Na Dkt. Nkwabi Sabasaba

ILIPOISHIA
MAISHA YA KAZI YA NDANI:
Hii ni nguvu yako ya ndani kama vile hamasa; hisia; imani; na unajisikiaje furaha yako. Maisha ya kazi ya ndani yanaweza kukufanya uifanye kazi kwa kiwango cha juu au cha chini, iwapo unafanya kazi ungali umevunjika moyo.
Nguvu ya kusonga mbele huchochewa na maisha ya kazi ya ndani kwa mujibu wa Dr. James Watts. Maisha ya kazi ya ndani yanaweza kuchochea kanuni ya maendeleo ifanye kazi pia.
Endelea...

Mabadiliko madogo madogo yanaweza kuchochea maisha ya kazi ya ndani. Mfano, mtaji wa sh. 5,000 au elfu kumi, utahusisha bidhaa ndogo ndogo ambazo kila mtu ana uwezo wa kuvinunua, na kwa kadri watu wanaponunua wengi kwa wakati mmoja, ndipo hamasa yako ya kuendelea kufanya biashara hiyo, inavyokua. Unapoona watu wengi wananunua bidhaa yako kwa wingi, japo ni ndogo, maisha ya kazi ya ndani yanaoongezeka. Unajiona umefanya jambo.
Mnamo mwaka 1983, Steve Jobs alikuwa akijaribu kumshawishi John Sculley aache kazi ya muhimu sana kwenye kampuni ya Pepsico ili awe Mkurugenzi Mkuu wa  Apple. Jobs anaripotiwa kumwambia, “Je, unapenda kuyatumia maisha yako yote yaliyobaki kuuza maji yaliyotiwa sukari, ama unataka nafasi ya kuubadili ulimwengu?”. Kauli hii ya Jobs inataka kutuambia kwamba kuna  kazi zenye maana. Kazi yenye maana ni ile ambayo italeta  mabadiliko kwa watu, na itatutia moyo kuona inavyoleta mabadiliko.

AINA SABA ZA IMANI-MAZOEA ZISIZO NA FAIDA, NA JINSI YA KUZITOA:
Mambo yanayotuzuia kusonga mbele ni imani zetu binafsi. Imani hizi zimezaliwa kutokana na sababu kwamba jambo hili tuna uzoefu nalo, au tumekuwa tukiambiwa, au kufundishwa. Watu waliofanikiwa ni wale walioamuru kukana imani hizo na kufanya kilicho mbele yao.
Mfano:
-        Kwa kuwa kitabu pekee ambacho hakina makwazo ni quran au biblia, maana yake ni kwamba kusoma vitabu vingine, nitakwazika.
-        Kuchagua tovuti (website) na kuzitembelea,  zingine huna mapenzi nazo.
-        Kuamini kuwa watu wafupi ni wabishi, kwa hiyo hupendi ushirika nao, n.k.
Ebu sasa tutazame aina za imani mazoea, ambazo hazina faida, na namna ya kuondokana nazo:

1. KUTEGEMEA KITU KUTOKA KWA WENGINE, AU KUTOKA MAISHANI:
Haimaanishi kwamba uache kushirikiana na wengine ili kupata mchango wao. Ukweli, wewe ndiyo kichocheo kikuu cha mabadiliko ya ulimwengu wako. Ijulikane kwamba mchango wa msaada wa watu kwako, ni kwa sababu ya juhudi zako. Watu hujitokeza zaidi kukusaidia kama umewakaribisha wakusaidie, au iwapo wameona juhudi zako. Pia, kitendo cha kuwakaribisha wakusaidie, hiyo ni juhudi yako. Juhudi yoyote huzaa matunda. Msemo ‘mtaji wa maskini ni nguvu zake mwenyewe’ , una maana kwamba wewe ndiye mtaji. Mtaji hauko pale wala huko, ila ni wewe mwenyewe. Jipe moyo mwenyewe, moyo ukiwa na hamasa, utafanikiwa.
Franklin D. Roosevelt alisema, ”Kipingamizi pekee cha mafanikio yetu ya kesho, ni ile hofu tuliyo nayo leo.”
Kila mtu kabla hajaanza kutenda, mafanikio yake ni 100%. Anapoanza kutenda, mafanikio yanaanza kupungua hadi 90% na kushuka chini, lakini hutegemea kila hatua ya utendaji wako unaambatanisha hofu kiasi gani.

2. KUTEGEMEA KUWAZA TU, NA KUPUUZA SAUTI YA NDANI:
Watu wengi hawatilii maanani hisia na sauti za ndani au kutoziamini. Kuna aina mbili za kuwaza. Kuwaza kwa akili ya ufahamu. Hii huwaza taratibu sana na inatumia nguvu nyingi. Na kuwaza kwa kutumia akili ya kina, hii huwaza kwa haraka sana. Akili ya fahamu hukuletea majibu yaliyofikiriwa kwa makini kisha, kuamriwa. Majibu hayo yapo katika mpangilio mahsusi, wakati akili ya kina hutumia imani, na majibu yake ni ya haraka.
Mfano, kuna familia moja ilikuwa inauza nyumba. Jirani yao  akasema ataleta mteja. Siku moja  kweli jirani akaleta mteja, familia ikakubaliana na mteja kuwa nyumba iuzwe kwa shilingi  milioni 70.
Itaendelea wiki ijayo.

Na Arone Mpanduka

Hivi karibuni tumeshuhudia Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) likimtimua kocha wa timu ya taifa (Taifa Stars), Kim Poulsen, baada ya kutoridhishwa na mwenendo wake ikiwemo Taifa Stars kupoteza kwenye mchezo wa nyumbani wa kuwania tiketi ya kufuzu fainali za Afrika kwa wachezaji wa ndani.
Wapo watu walioshangaa, na wapo walioona kuwa maamuzi yaliyofanywa ni sahihi kwa sababu kocha haajiriwi ili afukuzwe hasa kama ikitokea kushindwa jukumu alilopewa.
Kwa miaka mingi sasa tumekuwa tukiajiri makocha kwa timu ya taifa na kisha kuwatimua, huku tukiwashushia lawama nzito kwamba wao ndiyo sababu kuu ya timu zetu kushindwa. Mwaka 2006 Rais Jakaya Kikwete kwa wakati ule, alituonyesha njia kwa kumleta kocha wa kigeni Marcio Maximo kutoka nchini Brazil, na hapo ndipo tukawa tunaamini moja kwa moja kwamba suluhisho kuu la timu zetu za taifa kufanya vizuri ni kuajiri makocha wa kigeni.
Ninadhani kuna mahali tunakwama, na pengine hatufahamu suluhisho lake, na hata kama tunalifahamu, tunaamua kujifanya hatufahamu. Unapofanya jambo ambalo hujui, unakwenda wapi na ukaendelee kulilazimisha, itakuwa sawa na kufukuza kuku gizani, ukidhani utamkamata.
Ukweli ni kwamba mafanikio ya timu zetu za taifa yamekuwa yanapatikana kwa kubahatisha, na si katika mifumo sahihi. Bado tunaogopa kuanza na sifuri ili twende mbele, na badala yake tunataka kulazimisha, tukiamini kwamba tutafika tunapopataka.
Kuna vitu havipo sawa, na inabidi turekebishe ili soka letu lifike tunapopataka.Na vitu hivyo vinaanzia katika ngazi ya familia, Serikali na vyombo vinavyohusika na mchezo wa soka.
Tatizo kubwa tulilonalo ni kutokuwa na mfumo bora wa kufikia mafanikio ya mpira wa miguu, vinginevyo tutaishia kuilaumu TFF na makocha wanaokuja kufundisha timu zetu.
Tukianzia ngazi ya familia, wachezaji wote waliopo wana wazazi au walezi wao. Je, nini mchango wao katika malezi ya kimwili na kisaikolojia kwa watoto wao? Kwa sababu leo hii tunaweza kuwa na wachezaji wazuri wazawa lakini hawana nidhamu.
Kitu ambacho ni muhimu kwa maisha ya mchezaji kinachoweza kumpeleka nje ya nchi kucheza soka la kulipwa, na hatimaye kuongeza ubora kwenye timu za taifa, ni ufundi au umahiri wa kucheza soka.
Jambo lingine katika familia ni suala la lishe bora. Je, umewahi kujiuliza ni kwa nini wachezaji wa kizazi hiki wana maumbo madogo madogo, ikilinganisha na wale wa miaka 30 iliyopita? Wazazi katika hilo wanahusikaje?
Ukija katika ngazi ya klabu, je, vilabu vyetu vinaendeshwa kwa weledi, kwa maana ya kuandaa timu zetu za wakubwa? Kuna uwekezaji wa kiwango gani katika miundo mbinu ya soka?
Kwa sababu ukichunguza kwa makini utabaini, kwamba klabu chache za Ligi Kuu zina mifumo mizuri ya kutengeneza vijana, lakini zingine hazina, na hata yakitokea mashindano ya vijana, wanachofanya ni kuokota vijana wa mitaani ili kuiridhisha TFF.
Tukija kwa Serikali, je, kuna viwanja vingapi vya wazi ambavyo vilikuwa vinatumika kwa michezo zamani, lakini sasa hivi vimegeuzwa kuwa ofisi za watu binafsi, gereji, shule ama baa? Na katika hilo hilo la viwanja, ni shule ngapi za umma za Msingi na Sekondari zina viwanja vye michezo? Watoto watacheza wapi? Vipaji tutaviibua wapi? Na hapo ndipo msingi wa soka wa nchi yoyote unapoanzia.
Je, kuna waalimu wangapi wa michezo waliofuzu kwenye eneo hilo katika shule zetu za umma za msingi na sekondari, na je, kuna shule ngapi zenye vipindi na ratiba za michezo kama ilivyokuwa zaidi ya miaka 40 iliyopita?
Majibu ya jumla ni kwamba kwa sasa hakuna maeneo mengi ya wazi, na hata shule nyingi za umma ninazoziona mitaani hazina viwanja vya kuchezea. Mfano mzuri ni Shule ya Msingi Tabata Liwiti, ambayo ipo jirani kabisa na ofisi za Tumaini Media ambayo uwanja wake wa soka linajengwa jengo la Shule ya Sekondari. Pongezi kwa kuweka jengo hilo, lakini watoto watachezea wapi?
Hapo Wizara husika na Baraza la Michezo la Taifa (BMT) wanapaswa kutengeneza na kusimamia mfumo ulio bora ambao ndio utakuwa muongozo wa nchi. Nilisikia sera ya michezo inakamilishwa, lakini bado sifahamu ilipofikia.
Itaendelea wiki ijayo.

Baba Mtakatifu Fransisko (kushoto) akisalimiana na Baba Mtakatifu Mstaafu Benedikto XVI wakati Papa alipomtembelea Mstaafu huyo katika makazi yake, akiambatana na Makardinali wapya.

Vatican City

Makardinali Wapya wamemtembelea na kumsalimia Baba Mtakatifu Mstaafu Benedikto XVI, katika makazi yake.

Makardinali hao 20 walifanya ziara hiyo ya Kitume, baada ya Ibada ya kutangazwa na kusimikwa, ambapo walikwenda kumsalimia na kumtakia heri Baba Mtakatifu Mstaafu Benedikto XVI.

Mababa Watakatifu hao wawili kwa pamoja baada ya kusalimiana na kuteta na Makardinali hao wapya, waliwabariki ili wakawashe moto wa huruma na upendo wa Mungu kwa waja wake.

Baba Mtakatifu Fransisko aliwatangaza na kuwasimika Makardinali wapya na kuwapigia kura Wenyeheri wapya wanaotarajiwa kuingizwa kwenye orodha ya Watakatifu wa Kanisa.

Wenyeheri hao ni Mwenyeheri Padri Giovanni Battista Scalabrini aliyetangazwa na Mtakatifu Yohane Paulo II, kuwa Mwenyeheri, Novemba 9, mwaka 1997.
Padre Giovanni Battista alizaliwa Julai 8, mwaka 1839 na kufariki dunia Juni Mosi mwaka 1905.

Alikuwa ni Askofu wa Jimbo Katoliki la Piacenza-Bobbio, Italia na Mwanzilishi wa Mashirika ya Wamisionari wa Mtakatifu Carlo Borromeo, maarufu kama Wascalabrini, na pia ni Muasisi wa Taasisi ya Waamini Walei Wascalabrini, iliyoanzishwa kunako mwaka 1961.

Wa pili ni Mwenyeheri Artemide Zatti, Bruda wa Shirika la Wasalesian wa Don Bosco, aliyezaliwa tarehe 12 Oktoba 1880, nchini Italia.
Akafariki dunia Machi 15, mwaka 1951 huko Viedma nchini Argentina.

Utakatifu wake unapata chimbuko lake katika huduma kwa maskini kwa kuongoza hospitali na duka la dawa kwa ajili ya maskini, kwa muda wa miaka 40.
Aprili 14 mwaka 2002, alitangzwa na Baba Mtakatifu Yohane Paulo II, sasa ni Mtakatifu, kuwa ni Mwenyeheri.