Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Wakristo wahimizwa kufanya kazi kwa bidii

DODOMA

Na Ndahani Lugunya

Wakristo nchini wametakiwa kufanya kazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo, kuchangia Pato la Taifa, na kutatua changamoto katika maeneo yao.
Hayo yalielezwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu, George Simbachawene, wakati akizunguma katika sherehe ya kumweka wakfu Askofu wa  tatu wa Kanisa  la Anglikana, Dayosisi ya Mpwapwa, George Chiteto, iliyofanyika Jijini Dodoma, baada ya aliyekuwa Askofu wa Kanisa hilo, Askofu Donald Mtetemela kustaafu.
Simbachawene alisema kuwa changamoto nyingi za kiuchumi katika jamii zitatatuliwa endapo wananchi watajituma kufanya kazi na kuwa wabunifu  kwa kuanzisha miradi mbalimbali, kama ambavyo Maandiko Matakatifu yanavyoagiza watu kufanya kazi.
“Lazima Wakristo wa sasa tufanye kazi, lazima tutatue changamoto kwenye maeneo yetu kwa sababu imeandikwa katika Biblia, ‘asiyefanya kazi na asile’, kwa hiyo kufanya kazi ndio uhai wako, heshima yako na ukizalisha, utaweza kuendesha maisha yako binafsi,” alisema Simbachawene.
Aliongeza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na Taasisi za Dini, kwani zimekuwa na mchango mkubwa katika maendeleo, kusimamia maadili na kupambana na vitendo vya mmomonyoko wa maadili kwa baadhi ya watu wasio na hofu ya Mungu.
Aidha, alibainisha kwamba Serikali inaendelea  kuchukua hatua za kisheria kwa watu wote wanaojihusisha na vitendo vya rushwa, ufisadi, utovu wa nidhamu kwa watumishi wa umma, pamoja na jamii kwa ujumla.
Kwa upande wake Askofu Mkuu wa Kanisa Anglikana Tanzania, Dk. Maimbo  Mndolwa, aliipongeza Serikali kwa kuwa mstari wa mbele kuziunga mkono Taasisi za Dini  katika nyanja zote, huku akimtaka Askofu Chiteto kufanya kazi kwa kumtegemea Mungu, hatimaye kufikia malengo ya Kanisa.
Naye Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary  Senyamule  aliwataka wakazi wa mkoa huo kutumia fursa ya Serikali  kushusha bei ya  mbolea kwa kujikita katika kilimo.

Rate this item
(0 votes)
Last modified on Friday, 02 September 2022 15:05
Super User

Selfies labore, leggings cupidatat sunt taxidermy umami fanny pack typewriter hoodie art party voluptate. Listicle meditation paleo, drinking vinegar sint direct trade.

www.themewinter.com

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.