Nairobi, Kenya
Mwendesha baiskeli wa Kenya Suleiman Kangangi amefariki dunia kufuatia ajali ya mwendo kasi katika mbio za magari nchini Marekani siku ya Jumamosi.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 ambaye alikuwa akishiriki mbio za changarawe za Overland huko Vermont, shindano la kilomita 59 la barabara za udongo, likijumuisha takriban futi 7,000 za kupanda.
Kangangi alimaliza wa tatu katika Tour of Rwanda mwaka wa 2017 alipokuwa akikimbilia timu ya UCI Continental ya Ujerumani, Bike Aid, kabla ya kubadili mbio za changarawe.
Kwa upande wake Rachel Ruto, mke wa rais mteule William Ruto wa Kenya, alichapisha kwenye Twitter, “Sote tutamkosa kama mtu binafsi. Kenya imepoteza bingwa. Pumzika kwa amani Sule”.
Nayo taarifa ya klabu yake ilisema, “Sule ni nahodha wetu, rafiki, kaka. Yeye pia ni baba, mume na mwana”.