Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Maaskofu waunda Kamati ya Kitaifa

Kamati ya Uongozi wa Kitaifa ya Kushughulikia Mambo ya Kitume iliyoteuliwa na Baraza la Maaskofu Katoliki nchini Ethiopia, ikiwa katika picha ya pamoja.

ADDIS ABABA, Ethiopia

Baraza la Maskofu Katoliki nchini Ethiopia limeunda Kamati ya uongozi Kitaifa, ili kushughulikia changamoto mbalimbali za Kitume.
Maaskofu hao wamepitia masuala msingi ya Kitume ya Kanisa, fursa na changamoto katika mkutano wao wa kawaida wa 53, na kuunda Kamati ya Uongozi ya Kitaifa itakayofanyia kazi maandalizi ya Mpango Mkakati wa Miaka 10, ili changamoto zilizojitokeza wakati wa mkutano huo, ziweze kutatuliwa ipasavyo.
Kamati ya uongozi ya Taifa itaongozwa na Katibu Mkuu Mchungaji Abba Teshome Fikre, na itakuwa na wajumbe 10 wakiwemo Naibu Katibu Mkuu, maafisa na wakuu wa CMRS, na Mshauri wa ndani.
Kamati ya kitaifa tayari imeanza kazi yake ya kujadili Mchakato wa Mpango Mkakati, kuandaa mikakati ya utekelezaji na jukwaa la awali la uhamasishaji. Kwa kuzingatia hili katika wiki chache zilizopita, kamati imeandaa Mpango Kazi wa Miezi Sita ijayo.
Kuanzia Agosti 10 hadi 13, awamu ya kwanza ya kazi imekuwa ziara katika Majimbo mbalimbali, na maandalizi ya mpango wa kina yamefanyika katika Majimbo sita, ambayo ni pamoja na Jimbo Kuu Katoliki la Addis Ababa, Vikariati ya Meki, Jimbo Katoliki la Kitume la Vazi, Vikariati za Hawasa, Sodo, Hossana, Jimma-Bonga, na Eparchy ya Emdibir.
Katika mchakato huo, majadiliano mbalimbali yalifanywa na Maaskofu na viongozi husika kuhusu Mpango Mkakati huo.
Baadhi ya ajenda zilizoonyeshwa katika mjadala ni pamoja na Asili ya Mpango Mkakati wa kina wa Kanisa; Umuhimu wa Mpango Mkakati wa Miaka 10; Mchakato na Changamoto za Sasa za Huduma ya Dayosisi; Wajumbe wa Kamati ya uongozi ya dayosisi wakishirikiana na kamati ya Taifa.
Kwa kuongezea, mafunzo mafupi kuhusu itifaki za mawasiliano na jukwaa pepe, yalitolewa ili mawasiliano ya kazi zijazo yawe na ufanisi.
Majadiliano mengine yatafanyika katika maeneo ya Eparchy ya Bahirdar-Dessie, Vicariate ya Nekemet, na Dayosisi ya Gambella, na wawakilishi wa makuhani wa Eparchy of Adigrat watafanya mkutano huko Addis Ababa.
Mpango Mkakati wa Kanisa nzima ni mojawapo ya maelekezo ya kazi yanayofuata yaliyoamuliwa na Baraza la Maaskofu, Mpango Mkakati wa Miaka 10 wa Kanisa utatayarishwa kwa kuzingatia maono ya pamoja ya Kanisa, kwa kuzingatia huduma ya kichungaji, maendeleo ya kijamii. na maelekezo ya kiutawala ya Kanisa.
Mpango wa miaka 10, unatathmini mipango ya awali iliyofanywa na taasisi za Kanisa, pamoja na ile ambayo imeanzishwa na inayotekelezwa. Muda mfupi wa mipango mkakati, changamoto katika utekelezaji na ukosefu wa tathmini kwa wakati, ulielezwa kuwa sababu kuu za kutotekelezwa.
Kamati ya Uongozi iligawa Mpango Mkakati katika awamu nne za utekelezaji, na kuweka ukomo wa muda kwa kila moja. Hatimaye, Mpango Mkakati unalenga Mashirika ya Kanisa kufanya kazi pamoja kwa ajili ya maono ya pamoja ambayo yanasimamia utume na maadili ya Kanisa Katoliki.

Rate this item
(0 votes)
Last modified on Friday, 02 September 2022 09:36
Super User

Selfies labore, leggings cupidatat sunt taxidermy umami fanny pack typewriter hoodie art party voluptate. Listicle meditation paleo, drinking vinegar sint direct trade.

www.themewinter.com

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.