PARIS, Ufaransa
Klabu ya Paris Saint-Germain (PSG) ya Ufaransa, inataka kumsajili mshambuliaji wa Manchester United ya Uingereza, anayecheza kwa mkopo katika klabu ya Borussia Dortmund ya Ujerumani, Jadon Sancho.
PSG ilisema kuwa kuhusu raia huyo wa Uingereza, bado hakuna mbinu rasmi, lakini upande wa Ligue 1 umechunguza masharti ya makubaliano.
Juventus na Borussia Dortmund bado wana hamu ya kumsajili Sancho, ingawa kwa jinsi mambo yalivyo, hawawezi kufikia thamani ya United.
Sancho amerejea kwenye mazoezi na kikosi cha kwanza cha United na anatarajiwa kuwa sehemu ya kikosi kitakachosafiri kuelekea Marekani kwa ajili ya ziara ya kujiandaa na msimu mpya wa klabu hiyo.
Meneja wa Manchester United Erik ten Hag alifanya mkutano chanya na Sancho huko Carrington mapema mwezi huu, huku akilenga mchezaji huyo kushiriki kikamilifu katika maandalizi ya msimu mpya.