LONDON, England
Bingwa wa masumbwi mara mbili kwa upande wa wanawake Natasha Jonas, anatarajiwa kupanda ulingoni kupigania taji lake la nne la dunia mnamo Julai 1 mwaka huu.
Natasha atapambana na Kandi Wyatt raia wa Canada kuwania taji lililo wazi la IBF uzito wa welter kwenye pambano la linguini likiwakutanisha wakinadada Franchon Crews-Dezurn dhidi ya Savannah Marshall.
Jonas, ambaye tayari amejumuishwa katika orodha ya WBC, IBF na WBO uzito wa super-welterweight, atashuka kwenye uzani wa welter kupigana na Kandi Wyatt kuwania ubingwa wa IBF ulio wazi wa pauni 147.
Pambano hili la ubingwa ni pambano la kwanza kwa Natasha mwaka huu, kufuatia kupambana sana mwaka 2022 alipopanda daraja mara tatu na kunyakua mataji matatu ya dunia, akiwa na uzito wa pauni (ratili) 154.
Mchezo huo ulimfanya awe mwanamke wa kwanza kutwaa taji la Bondia Bora wa Mwaka wa Uingereza katika tuzo za kila mwaka za Bodi ya Ndondi ya Uingereza.