Print this page

Makardinali waanza Mkutano Mkuu

VATICAN City

Mkutano Mkuu wa kwanza wa Makardinali umeanza Aprili 22 mwaka huu, ikiwa ni siku moja baada ya kifo cha Baba Mtakatifu Fransisko.
Mkutano huo ulidumu kwa muda wa saa moja na nusu, ambapo Makardinali waliokuwepo katika Ukumbi wa Sinodi mpya walikuwa 90, walioanza kikao hicho kwa muda wa sala kwa ajili ya Papa Fransisko.
Makardinali hao waliapa kwa kuzingatia na kwa uaminifu kanuni za Katiba ya Kitume (Universi Dominici Gregis), kuhusu nafasi ya Kiti kilicho wazi cha Kitume na kuchaguliwa kwa Papa wa Roma, kasha wakaimba (Adsumus Sancte Spiritus), wimbo wa kumuomba Roho Mtakatifu awaangazie.

Rate this item
(0 votes)
Japhet