Print this page

‘Wakatoliki hawaabudu sanamu’

By September 19, 2025 37 0
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi, akiondoka katika viwanja vya Kituo cha Hija Pugu, baada ya Adhimisho ya Misa Takatifu ya Kutukuka kwa Msalaba iliyoadhimishwa hivi karibuni jimboni humo. (Picha na Yohana Kasosi) Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi, akiondoka katika viwanja vya Kituo cha Hija Pugu, baada ya Adhimisho ya Misa Takatifu ya Kutukuka kwa Msalaba iliyoadhimishwa hivi karibuni jimboni humo. (Picha na Yohana Kasosi)

Dar es Salaam

Na Mathayo Kijazi

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi, ametoa ufafanuzi na kukanusha kwamba si kweli kwamba Wakatoliki wanaabudu sanamu, bali wanamwabudu Bwana Yesu Kristo, aliyejinyenyekesha, akatii mpaka kufa msalabani.
Aliyasema hayo hivi karibuni, katika homilia yake wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu, ya Sikukuu ya Fumbo la Kutukuka kwa Msalaba, iliyofanyika katika kituo cha Hija – Pugu, jimboni humo.

Rate this item
(0 votes)
Japhet