Print this page

Tatizo ulemavu wa macho kudhibitiwa

By September 19, 2025 42 0
Madaktari na Wataalamu wa Afya wakihudumia wagonjwa kwa ushirikiano kati ya Wizara ya Afya kupitia Mpango wa Taifa wa Huduma za Macho na Helen Keller International. Madaktari na Wataalamu wa Afya wakihudumia wagonjwa kwa ushirikiano kati ya Wizara ya Afya kupitia Mpango wa Taifa wa Huduma za Macho na Helen Keller International.

Mbozi

Na Mwandishi Wetu

Katika hatua muhimu ya kupunguza upofu, Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya (MZRH) na Shirika la Helen Keller International, leo wamewasili mkoani Songwe kwa ajili ya kutoa Huduma Mkoba ya matibabu ya ugonjwa wa mtoto wa jicho “Cataract Management”, kwa wananchi takribani 700 wa Songwe, katika Hospitali ya Wilaya ya Mbozi (Vwawa).
Akiongea na Waandishi wa Habari, Dk. Jofrey Josephat Mratibu wa Huduma za macho Mkoa wa Songwe, alieleza kuwa kambi hiyo ya siku sita imelenga kukabiliana na magonjwa ya mtoto wa jicho, na kusogeza huduma hizo adimu katika maeneo ya karibu na wanapoishi (vijijini), ambapo imekuwa ngumu kupatikana na gharama kwa wananchi, kuzifuata katika hospitali kubwa.

Rate this item
(0 votes)
Japhet