Print this page

Askofu Mkuu Rugambwa afariki Dunia

By September 19, 2025 48 0
Askofu Mkuu Novatus Rugambwa Askofu Mkuu Novatus Rugambwa

Bukoba

Na Mwandishi wetu

Balozi na Mwanadiplomasia wa Vatican, Mhashamu Askofu Mkuu Novatus Rugambwa ambaye ni Mtanzania, amefariki Dunia Jumanne ya Septemba 16, mwaka huu mjini Roma nchini Italia.
Taarifa iliyotolewa na Askofu wa Jimbo Katoliki la Bukoba Mhashamu Jovitus Mwijage  kwa Maaskofu, Mapadri, Watawa na Waamini ilieleza kwamba Askofu Mkuu Rugambwa aliaga Dunia wakati akipatiwa matibabu kutokana na changamoto za kiafya.

Rate this item
(0 votes)
Japhet