Zanzibar
Na Mwandishi Wetu
Tume ya Ushindani (FCC) na Tume ya Ushindani wa Haki Zanzibar (ZFCC), zimetia saini mkataba wa ushirikiano wenye lengo la kuhakikisha masoko yanakuwa na ushindani wa haki, na kulinda maslahi ya walaji nchini.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Tanzania Bara, Dk. Hashil Abdalah, alisema kwamba makubaliano hayo yameweka misingi muhimu, ambayo pande zote mbili zinapaswa kuizingatia katika utekelezaji.