Dar es Salaam
Na Mwandishi Wetu
Katika hali ya mateso na mahangaiko ya muda mrefu, kwa baadhi ya Mataifa ya Afrika, ambayo yalitumbukia kwenye mikono ya vita vya wenyewe kwa wenyewe, sasa mataifa mengi yameanza kutaka kujinasua kwenye mikono ya vita na vurugu za hapa na pale.
Kwa sasa dunia inashuhudia hali mbaya ya vita na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe, katika Mataifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Sudan Kusini na Sudan, bila kusahau huko Gaza ukanda wa Mashariki ya Kati.