Dar es Salaam
Na Mathayo Kijazi
Imeelezwa kuwa imani ya kweli si kujisifia, kujivuna, wala kujiona, bali kujishusha.
Hayo yalisemwa na Monsinyori Novatus Mrighwa, Mwalimu wa Seminari Kuu ya Mtakatifu Karoli Lwanga – Segerea, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakati wa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti ya Kipaimara, katika Parokia ya Mtakatifu Gaudance - Makoka, jimboni humo.