Print this page

Monsinyori: Imani ya kweli si kujisifia

Monsinyori Novatus Mrighwa wa Jimbo Kuu la Katoliki la Dar es Salaam, akizindua Groto la Bikira Maria katika Parokia ya Mtakatifu Gaudance - Makoka jimboni humo, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti ya Kipaimara. Kulia kwa Monsinyori ni Paroko wa Parokia hiyo Padri Amaradoss Chinappann na kushoto ni Paroko Msaidizi Padri Desiderius Rugemalira. (Picha na Yohana Kasosi) Monsinyori Novatus Mrighwa wa Jimbo Kuu la Katoliki la Dar es Salaam, akizindua Groto la Bikira Maria katika Parokia ya Mtakatifu Gaudance - Makoka jimboni humo, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti ya Kipaimara. Kulia kwa Monsinyori ni Paroko wa Parokia hiyo Padri Amaradoss Chinappann na kushoto ni Paroko Msaidizi Padri Desiderius Rugemalira. (Picha na Yohana Kasosi)

Dar es Salaam

Na Mathayo Kijazi

Imeelezwa kuwa imani ya kweli si kujisifia, kujivuna, wala kujiona, bali kujishusha.
Hayo yalisemwa na Monsinyori Novatus Mrighwa, Mwalimu wa Seminari Kuu ya Mtakatifu Karoli Lwanga – Segerea, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakati wa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti ya Kipaimara, katika Parokia ya Mtakatifu Gaudance - Makoka, jimboni humo.

Rate this item
(0 votes)
Japhet