Mahenge
Na Mathayo Kijazi
Askofu wa Jimbo Katoliki la Mahenge, Mhashamu Agapiti Ndorobo, amesema kuwa kuelekea katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, ni vyema kuchagua kiongozi anayefaa na anayejali kila mmoja, bila kuangalia dini, rangi, kabila, wala utaifa wake.
Askofu Ndorobo aliyasema hayo hivi karibuni, wakati wa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Jubilei ya Miaka 75, ya Seminari ya Mtakatifu Francis – Kasita, jimboni humo.