Print this page

Pawasa azitaka Klabu kuacha woga kimataifa

By November 07, 2025 37 0
Boniface Pawasa Boniface Pawasa

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Beki wa zamani wa timu ya Taifa Stars, Simba, CDA na Azam FC, Boniface Pawasa amezitaka timu nne zinazoshiriki hatua ya makundi ya michuano ya kimataifa ngazi ya klabu kuondoa woga.
Pawasa ametoa ushauri huo zikiwa ni siku chache zimepita tangu timu za Simba, Yanga, Azam FC na Singida Black Stars kuwafahamu wapinzani itakaokutana nao katika hatua ya makundi ya michuano ya Ligi ya Mabingwa na Shirikisho Afrika.
Akizungumza na Tumaini Letu, Pawasa alisema hivi sasa soka la Afrika limebadilika sana tofauti na ilivyokuwa miaka ya zamani, hivyo kila timu ijiandae kupambana vilivyo ili kwenda hatua ya robo fainali.

Rate this item
(0 votes)
Japhet