Manchester, Uingereza
Cristiano Ronaldo amesema Meneja wa Manchester United Ruben Amorim hatofanya miujiza kwa sababu kwa sasa klabu haipo katika njia nzuri.
Mshambuliaji huyo wa Ureno mwenye umri wa miaka 40 alijiunga na Al-Nassr muda mfupi baada ya kumaliza kipindi chake cha pili akiwa na United mnamo Novemba 2022.
Mchezaji mwenzake wa zamani wa Ureno, Amorim alichukua nafasi ya Erik ten Hag kama bosi mnamo Novemba 2024 na United ikamaliza msimu uliopita katika nafasi ya 15 kwenye Ligi ya Premia ukiwa mwisho wao mbaya zaidi wa ligi tangu washushwe daraja kutoka ligi kuu mnamo msimu wa 1973-74.