Miami, Marekani
Pambano la maonyesho la Jake Paul dhidi ya Bingwa wa Dunia wa uzani wa lightweight Gervonta Davis limeahirishwa.
Pambano hilo, lililopangwa kufanyika Novemba 14 mwaka huu huko Miami, lilipangwa kutikisa vichwa vya habari duniani kupitia Netflix.
Uamuzi huo unakuja siku chache baada ya kesi kufunguliwa dhidi ya Davis na mpenzi wake wa zamani akimshtaki kwa unyanyasaji wa kijinsia, utekaji nyara na kuumiza hisia kwa kukusudia.