Print this page

Wazazi warithisheni watoto Imani Katoliki

By November 07, 2025 47 0
Paroko wa Parokia  ya Mtakatifu Augustino-Salasala, Jimbo Kuu Katoliki la Dar  es Salaam, Padri Peter Assenga (kushoto), akimbatiza mmoja wa watoto wa parokia hiyo, wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti ya Ubatizo na Ekatisti. (Picha na Yohana Kasosi) Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Augustino-Salasala, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Peter Assenga (kushoto), akimbatiza mmoja wa watoto wa parokia hiyo, wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti ya Ubatizo na Ekatisti. (Picha na Yohana Kasosi)

DAR ES SALAAM

Na Mwandishi wetu

Waamini wametakiwa kufuata mafundisho ya Bwana Yesu Kristo na mwenendo wake, kwa kuwarithisha watoto wao Imani Katoliki.
Wito huo ulitolewa hivi karibuni, na Paroko wa Parokia  ya Mtakatifu Augustino-Salasala, Jimbo Kuu Katoliki la Dar  es Salaam, Padri Peter Assenga, wakati akitoa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti ya Ubatizo na Ekatisti.
“Mkristo kamili lazima awe amebatizwa na mwenye kushiriki Ekaristi Takatifu, na kufanya maungamo mara kwa mara,” alisema Padri Assenga.
Aidha, aliwasihi Waamini kutopokea Ekaristi Takatifu kama pipi, kwa sababu ni kufuru na ni dhambi.

Rate this item
(0 votes)
Japhet