Print this page

‘Msijiruhusu kuwa karakana ya shetani’

By November 07, 2025 58 0
Waamini wakiwa kanisani wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika. (Picha na Yohana Kasosi) Waamini wakiwa kanisani wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika. (Picha na Yohana Kasosi)

Dar es Salaam

Na Laura Mwakalunde

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi, amewaonya Waamini kutoruhusu wao kuwa karakana ya shetani.
Alisema hayo katika Adhimisho la Misa Takatifu ya uzinduzi wa nyumba ya Mapadri, iliyofanyika katika Parokia ya Bikira Maria wa Consolatha-Mbezi Makabe.
“Kila Mkristo inampasa kuwa na maamuzi kwa kuachana na mambo ya kale, aibu ya giza, kwani inasikitisha kuona Mkristo anakwambia bado kidogo,” alisema Askofu Mkuu Ruwa’ichi.
Aidha, aliwataka Waamini watambue kuwa wao ni warumi wa leo, kwa sababu Mtume Paulo huwa anafundisha ukweli wa mambo ya kale, ya aibu na ya giza, kwa kutoruhusu akili na utashi wao kuwa kichaka cha dhambi.

Rate this item
(0 votes)
Japhet