Dar es Salaam
Na Mwandishi wetu
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi OFMCap, amesema kuwa hakuna amani bila haki, kwani haki ni msingi wa lazima wa amani.
Askofu Mkuu Ruwa’ichi alisema hayo katika Adhimisho la Misa Takatifu, ya Kuwaombea watu waliouawa katika wiki ya Uchaguzi Mkuu Tanzania, iliyoadhimishwa hivi karibuni, katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu, jimboni humo.