Print this page

Zaka Zakazi aondoa utata mabao ya Stars

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Mkuu wa Kitengo cha Habari cha klabu ya soka ya Azam FC, Thabit Zacharia maarufu kama Zaka Zakazi, amesema kuwa kitakwimu winga wa Taifa Stars Simon Msuva, bado ataendelea kuwa juu katika ufungaji wa mabao mengi katika kikosi hicho, kuliko mchezaji mwingine yoyote.
Akitoa ufafanuzi kuhusiana na ubishani unaoendelea, wa kumlinganisha Msuva na mchezaji wa zamani wa Taifa Stars Mrisho Ngassa, Zaka alisema kwamba nyota hao wanalinganishwa kimakosa, kwa sababu Msuva ana mabao 21 aliyoifungia Taifa Stars pekee, huku Ngassa mabao yake yakichanganywa na aliyoifungia Kilimanjaro Stars, ambayo ni ya Tanzania Bara pekee.

Rate this item
(0 votes)
Japhet