DAR ES SALAAM
Na Nicholas Kilowoko
Kocha wa vijana wa klabu ya soka ya Simba, John Bocco, ameelezea mikakati yake mipya ya kuisaidia timu yao kubwa, kupata vijana wazawa wenye vipaji na watakaolisaidia Taifa pia.
Kwa muda mrefu nyota huyo wa zamani, ambaye alifanya makubwa ndani ya klabu ya Simba, Azam FC, na JKT Tanzania, alikuwa yupo kimya mara baada ya kumaliza kazi yake ya uchezaji.