Print this page

Kanisa Msumbiji lapata Jimbo, Askofu mpya

MAPUTO, Msumbiji

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Ulimwenguni, Baba Mtakatifu Leo XIV ameunda Jimbo Jipya la Caia (Dioecesis Caiana), nchini Msumbiji, na kumteuwa Askofu Msaidizi António Manuel Bogaio Constantino, M.C.C.J., wa Jimbo Kuu Katoliki la Beira, nchini humo, kuwa Askofu wake wa kwanza.
Jimbo la Caia limeundwa baada ya Baba Mtakatifu Leo XIV kumega Jimbo Kuu Katoliki la Beira, Jimbo Katoliki la Chimoio, Quelimane na Jimbo Katoliki la Tete, huku Jimbo hilo jipya likiwa na Parokia 16, Mapadre wa Jimbo 15, Watawa wa kike 17, na Waseminari 18.
Kwa mujibu wa Vatican News, lengo la Mama Kanisa kuunda Majimbo mapya ndani ya Kanisa Katoliki, kunalenga kusogeza huduma za kiroho na kichungaji kwa watu wa Mungu.

Rate this item
(0 votes)
Japhet