Print this page

Askofu Ruwa’ichi: Mwaka 2025 ulikuwa wa majonzi

Dar es Salaam

Na Laura Mwakalunde

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi amewataka watawa kufamu kuwa mwaka 2025, ulikuwa wa neema na majonzi.
Askofu Mkuu Ruwa’ichi alisema hayo hivi karibuni wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Nadhiri za Masista wa Shirika la Mtakatifu Fransiko wa Asizi Dada Wadogo, iliyofanyika katika Nyumba Kuu ya Shirika hilo -Mbagala jimboni humo.
“Mwaka 2025 ulikuwa ni mwaka wa neema kwa sababu ndiyo mwaka pekee wa Jubilee Kuu, japo ulikuwa ni mwaka wa majonzi, masikitiko na vifo ila Mungu hakutuacha wala kututupa kwani ndiye tegemeo na kimbilio,”alisema Askofu Mkuu Ruwa’ichi.

Rate this item
(0 votes)
Japhet