DAR ES SALAAM
Na Mwandishi wetu
Shirikisho la ngumi Tanzania (BFT), limeandaa mikakati ya kumleta bondia maarufu duniani, Manny Pacquiao, nchini Tanzania, kwa ajili ya mashindano ya semi Pro fights ya BFT.
Lengo la BFT kumleta Pacquiao nchini Tanzania, ni kwa ajili ya uzinduzi wa mashindano hayo, pia atashiriki matukio ya kijamii ya kuinua mchezo wa ngumi hapa nchini.