DAR ES SALAAM
Na Mathayo Kijazi
Wakristo wamesisitizwa kuwa wanakanisa halisi, hasa katika zama hizi zenye ugeugeu na ubabaishaji mwingi, ili waendelee kuwa na roho zenye uadilifu na uungwana.
Kauli hiyo ilitolewa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi, wakati wa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Jubilei ya Miaka 25, ya Parokia ya Bikira Maria Mkingiwa Dhambi ya Asili - Mavurunza, jimboni humo.