DAR ES SALAAM
Na Angela Kibwana
Zaidi ya shilingi milioni 200, zinatarajiwa kutumika katika ujenzi wa nyumba ya Padri, katika Parokia mpya ya Bikira Maria wa Rozari-Msomwero, jimboni Morogoro, ambayo itakuwa ni hatua muhimu ya kukamilisha makazi ya Padri, anayefanya utume parokiani hapo, kwa lengo la kusogeza huduma za kiroho kwa Waamini.
Akizungumza kwa mahojiano maalumu, Paroko wa Parokia hiyo Padri Chediel Mloka, amebainisha kuwa parokia hiyo mpya ilitangazwa miaka mitatu iliyopita, na Askofu Lazarus Vitalis Msimbe SDS, wa Jimbo Katoliki Morogoro, ili kunusuru imani za Waamini ambao walikuwa wanapata huduma za kiroho, katika Parokia ya Ilonga.
Alisema kuwa kwa sasa wakati anaendelea kusubiri kukamilika kwa nyumba hiyo, anaishi nyumba ya kupanga umbali wa Kilomita nne toka yalipo makazi hayo, hadi kufika kanisani hapo.