DAR ES SALAAM
Na Mathayo Kijazi
Abate Christian Temu –OSB wa Abasia ya Ndanda, Jimbo Katoliki la Mtwara, amesema kuwa maisha ya Mkristo ni kama Hija, kwani kila wakati anakuwa safarini kuelekea mbinguni kwa Mwenyezi Mungu.
Aidha, Abate Temu amewasihi Wakristo kutoogopa jambo lolote, akiwasihi kuwa majasiri kwani Mungu yupo nao, na masuala ya amani na haki ni matunda ya Kimungu.
Abate Temu alitoboa siri hiyo hivi karibuni katika homilia yake, katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Kufunga Jubilei ya Miaka 2025 ya Ukristo, iliyoadhimishwa katika Kituo cha Hija - Pugu, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam.