GULU, Uganda
Maandalizi ya kutangazwa Padri Joseph Ambrozoli kuwa Mwenyeheri yanaendelea vizuri, tukio litakalofanyika wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu itakayofanyika Jimbo Kuu Katoliki la Gulu, Uganda Novemba 20, mwaka huu.
Mchungaji John Baptist Odama wa Jimbo Kuu Katoliki la Gulu alisema kuwa Kamati Kuu ya Maandalizi (COC) yenye kamati ndogo 16 imeundwa, na wote wanafanya kazi ya kuona jinsi ya kuwapokea watu watakaokuja kuhudhuria ibada hiyo.