Dar es Salaam
Na Laura Mwakalunde
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi, amewaonya Waamini kuacha kuwa Wakristo goigoi.
Aliyasema hayo hivi karibuni, wakati akitoa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti Takatifu ya Kipaimara, iliyofanyika Parokia ya Bikira Maria wa Fatima-Msimbazi, jimboni humo.