Dar es Salaam
Na Mwandishi Maalumu
Watanzania wametakiwa kujenga utamaduni wa kupima afya zao mara kwa mara, hasa magonjwa yasiyo ambukiza, ili kuepuka madhara zaidi.
Rai hiyo ilitolea hivi karibuni, na Daktari Bingwa wa magonjwa ya ndani kutoka Taasisi ya Saratani Ocean Road, jijini Dar es Salaam, Dk. Kezia Tessua, wakati akizungumza na Wananchi katika eneo la Bunju, kwenye Programu ya Viongozi Wanawake, inayosimamiwa na Taasisi ya Uongozi.