Visiga
Na Laura Mwakalunde
Makamu wa Askofu wa Jimbo Katoliki la Bagamoyo, Padri Edward Sabbas amesema kwamba, Taifa linaloshindwa kufuata misingi bora ya utu hupotoka.
Padri Edward alisema hayo hivi karibuni, wakati akihubiri katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Mahafari ya Kidato cha Nne, katika Seminari Ndogo ya Maria –Visiga, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam.