Print this page

Askofu awanyoshea kidole wenye nia ovu

Shinyanga

Na Angela Kibwana

Mhashamu Askofu Liberatus Sangu wa Jimbo Katoliki la Shinyanga, amewata Wakatoliki kuendelea kuombea na kulinda amani ya nchi, hasa kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Jumatano Oktoba 29 mwaka huu, ili uwe huru na haki.
Askofu Sangu alisema hayo, wakati akihubiri katika Adhimisho la Misa Takatifu, iliyofanyika Parokia ya Mt. Rosa wa Lima – Kitangili jimboni humo, akiwakumbusha Wakatoliki kumuomba Mama Bikira Maria, alinde familia zao na Taifa kwa ujumla kuelekea Uchaguzi Mkuu, kabla na baada ya uchaguzi huo.

Rate this item
(0 votes)
Japhet