DAR ES SALAAM
Na Nicholausi Kilowoko
Timu ya Umoja wa Maveterani wa Soka Tanzania (UMSOTA), imeahidi kuendelea kushiriki mashindano mbalimbali ndani na nje ya nchi, kwa lengo la kuimarisha umoja na kukuza michezo.
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa UMSOTA, Paul Ambrose Lusozi maarufu kama Father, huku akiishukuru serikali kwa kutambua mafanikio yao kimataifa.
Timu hiyo ilitwaa ubingwa wa mashindano ya soka ya Maveterani Afrika Mashariki, yaliyofanyika Oktoba mosi mwaka huu, huko nchini Kenya.