Print this page

Miundombinu ya Kanisa kuanzia Karne ya nne

By November 07, 2025 34 0

Katika safu hii ya Chimba Chimba Historia ya Kanisa wiki iliyopita, tuliendelea kuwaletea historia ya kuibuka kwa Dola ya Kikristo, hususani tuliwajuza kuhusu Faida na Hasara za Dola ya Kikristo. Leo tunawaletea historia ya Miundombinu ya Kanisa kuanzia Karne ya nne na tano. Sasa endelea…

Watumishi wa Kanisa na Mitaguso:
Bwana wetu Yesu Kristo, aliacha amewachagua na kuwaweka mitume 12 na wafuasi 70 (72), ili waendeleze kazi aliyoianza (Lk. 6:13-16; 10:1-12). Hawa walirithiwa kama Maaskofu na Mapadri.
Katika Kanisa la mwanzo, polepole kufuatana na mahitaji katika misingi aliyoiweka Kristo, miundombinu hiyo iliongezeka na kuboreshwa.
Kuanzia Karne ya nne na tano, palikuwepo na madaraja saba katika watumishi wa Kanisa. Kati ya madaraja hayo, madogo ni manne yakiwemo Mfungua Mlango, Msomaji, Mtoa Mashetani na Mtumishi wa Ibada, na madaraja makubwa ni matatu, Ushemasi, Upadri na Uaskofu.

Rate this item
(0 votes)
Japhet

Latest from Japhet