Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha
Makala

Makala (67)

Na Mwandishi Wetu

Katika makala haya kuhusu Ubatizo wa Bwana, Mwadhama Protace Kardinali Rugambwa katika mahubiri yake, ametumia fursa hii kufafanua alama muhimu, zilizojionesha wakati Kristo Yesu alipobatizwa mtoni Yordani.

Anasema kwamba alama ya kwanza ni Maji: Alama ya kifo na uhai; Mbingu zikamfunukia, Roho Mtakatifu akashuka juu yake kama hua; Alama ya pili ni kufunguka kwa mbingu; Alama ya mabadiliko ya ndani ya mwanadamu, mbele ya Mwenyezi Mungu; Alama ya tatu ni Roho Mtakatifu aliyemshukia Kristo Yesu na sauti ya Baba wa milele ikasikika: Huyu ni mwanangu, mpendwa wangu.

Ubatizo ni sakramenti inayotuingiza katika Ukristo, ni sakramenti inayotuondolea dhambi ya asili na adhabu zake zote. Ni kwa njia ya Ubatizo tunazaliwa upya kwa maji na Roho Mtakatifu, na hivyo tunakuwa ni watoto wa Mungu na wa Kanisa.

Na Dkt. Felician B. Kilahama

Namshukuru Mwenyezi Mungu aliye mwingi wa rehema, aliyeumba wanadamu kwa sura na mfano wake. Hili ni “wazo mbadala”, ikimaanisha kwamba kuna kinachotakiwa kufanyika, lakini katika harakati za utekelezaji likajitokeza ‘wazo mbadala’.
Uchaguzi Mkuu ulifanyika Oktoba 29, 2025, na aliyekuwa mgombea urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Mheshimiwa Dk. Samia Suluhu Hassan, akatangazwa mshindi na kuapishwa rasmi Jumatatu, Novemba 3, 2025.
Baada ya zoezi hilo kukamilika, Rais aliunda Baraza la Mawaziri, ambalo pamoja na Wakuu wa Mikoa, Wilaya, Viongozi wakuu wa Halmashauri husika, kwa pamoja inakuwa Serikali inayoongozwa na Rais.
Wakati wa kampeni za uchaguzi, kuna sehemu ambazo wananchi waliomba serikali itakayoundwa, kuanzisha wilaya na halmashauri mpya, ili kuwarahisishia wananchi kupata huduma wanazohitaji, ikiwemo kutatuliwa kero haraka iwapo ofisi husika zitakuwa karibu.

Dar es Salaam

Na Dk. Felician B. Kilahama

Mapokeo ya kihistoria tangu miaka ya 1880, yanathibitisha kwamba baadhi ya mataifa barani Ulaya mathalani, Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Ubelgiji na Hispania, yaliweza kufika barani Afrika.
Hivyo, 1884 kukafanyika kikao maalumu jijini Berlin-Ujerumani, kwa lengo mahususi kugawana maeneo kuitawala Afrika.
Kwa upande wa Afrika-Mashariki, Wajerumani wakatawala “Tanganyika” na wakaweza kufika maeneo ya Iringa, ambako Hifadhi-Ruaha inapatikana. Wakiwa huko waliona sehemu imesheheni rasilimali nyingi za wanyamapori, na kuifananisha na “Bustani ya Edeni”.
Kiuhalisia Ruaha kuna urithi wa aina yake, mathalani milima na mabonde pamoja na rasilimali-misitu aina ya miombo, misitu inayostawi kandokando ya mito, na Mto Ruaha-Mkuu. Mto huu ni msaada mkubwa aina yake, ikiwemo wanyamapori wanaoishi kwenye hifadhi ya Ruaha.

MWANZA

Na Paul Mabuga

Hebu vuta picha: Zamani kijana wa Kitanzania hakukurupuka tu kuitwa mzazi. Kulikuwa na mifumo madhubuti ya Jando, Unyago, na yale mafunzo ya kando ya moto kutoka kwa babu na bibi, yaliyomjenga mtu kifikra na kihisia. 
Lakini leo, “moto” pekee unaowaunguza vijana wetu ni wa data za simu, na mianga ya mitandao ya kijamii. Wakati mifumo hiyo ya kijadi ikipumzika kwenye makaburi ya historia, tunapaswa kujiuliza kwa uchungu: Je, vijana wetu wanajifunza wapi kuwa wazazi?

Dar es Salaam

Na Joseph Mihangwa

Chimbuko la Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni Mapinduzi ya Zanzibar, yaliyofanyika Visiwani humo Januari 12, 1964. 
Bila Mapinduzi hayo tusingezaliwa Tanzania, wala Chama tawala cha sasa - Chama cha Mapinduzi (CCM), ambacho ni Muungano wa Vyama vya Tanganyika African National Union (TANU) cha Tanganyika, na Afro-Shirazi Party (ASP) cha Zanzibar.
Chama kilichozaliwa Februari 5, 1977, miaka 13 baada ya Muungano uliofikiwa Aprili 26, 1977, ni matokeo ya kero za Muungano.
Mapinduzi haya yaliyoshangaza dunia kwa staili yake, yalifanyika kwa harakati za siasa za mrengo wa Kikomunisti, na kutia hofu nchi za Magharibi, hasa Marekani na Uingereza, zikaamua kuingilia kati kuyadhibiti Mapinduzi hayo, kuzuia kuenea kwa Ukomunisti Afrika kupitia Afrika Mashariki.

Katika safu hii ya Chimba Chimba Historia ya Kanisa wiki iliyopita, tuliendelea kuwaletea historia ya mitaguso mikuu, kwa kuendelea na Mtaguso Mkuu wa Kostantinopole. Leo tunawaletea historia ya kuasi kwa Kanisa la Wakopti Misri, na historia ya Mababa wa Kanisa wa Magharibi. Sasa endelea…

Bahati mbaya, Wakristo wa Misri ambao kabla walikuwa kila mara wanashinda, na hivyo wakajiona kama watetezi imara wa imani, mara hii waliposhindwa hawakufurahi. Walishinda wakati wa Arius na walishinda wakati wa Nestorius, lakini sasa kwa kusisitiza mno umoja na umungu wa Kristo walishindwa. 

Hawakupokea kushindwa, hivyo Kanisa zima likaendelea na uzushi huo ulioitwa ‘Monophysitism’, maana yake Yesu  ni Mungu na utu wake umekandamizwa. 

Mwanza

Na Paul Mabuga

Maandishi yaliyoandikwa kwenye bajaji zetu, ambayo  kwa  muhtasari na kwa  muktadha wa yaliyokusanywa katika makala haya, unaweza kusema ni kama kutoka, “Enzi za Mwalimu” hadi “Kwenye Ndoa Yenu...”:, na vilevile ni maneno yanayosema mengi yenye kusisimua, kuibua hisia, kufurahisha na hata kufikirisha, sembuse kutia hofu na kuogofya.

Ni kwamba licha ya barabara za miji yetu hapa nchini, kujaa watu na shamrashamra za kelele za honi, lakini  pia zimesheheni  falsafa ya Mswahili.. Sio kwenye vitabu au kwenye mikutano ya hadhara, bali kwenye mabango madogo yaliyobandikwa, au kuandikwa nyuma ya magari yetu ya usafiri, na vyombo vingine maarufu kama Bajaji.

Dar es Salaam

Na Pd. Richard Mjigwa- C.PP.S

Ilikuwa ni Novemba 8, mwaka 1984, Mtakatifu Yohane Paulo II (Papa), alipochapisha Waraka unaojulikana kama “Tot tantaeque” yaani “Bikira Maria ameidhinishwa kuwa Mlinzi na Mwombezi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania”, Sherehe inayoadhimishwa kitaifa kila mwaka ifikapo Desemba 9.
Katika mkesha wa uhuru wa Tanganyika, Mtakatifu Yohane XXIII, alitunga Sala Maalumu kwa ajili ya kuiombea Tanganyika, ili uhuru wake uweze kuwanufaisha watu wake.

DAR ES SALAAM

Na Edvesta Tarimo

Afya ya akili ni moja ya vipengele muhimu zaidi vya ustawi wa binadamu, lakini mara nyingi hupewa nafasi ndogo katika mjadala wa afya. 
Hata hivyo utafiti unaonesha kwamba, afya ya akili inajumuisha hali ya kiakili, kihisia na kijamii ya mtu, na ni msingi wa jinsi anavyokabiliana na changamoto za kila siku. 
Licha ya kwamba kila mtu anapitia magumu maishani, kuna njia za kujikinga dhidi ya athari za majeraha ya kihisia (kiwewe), na kujenga uthabiti wa kukabiliana na hali ngumu.

DAR ES SALAAM

Na Shemasi George Timalias

Karibu ndugu msikilizaji wa Radio Vatican, katika tafakari hii, inayotugusa kwa karibu sana, ambayo inakumbusha Sikukuu ya Watakatifu wote, kila ifikapo tarehe Mosi Novemba ya kila mwaka, lakini pamoja na Watakatifu, kuna ndugu zetu Marehemu wote waliotutangulia mbele ya haki, ambapo Mama Kanisa anatupatia fursa ya kuwakumbuka, kila ifikapo  tarehe 2 ya mwezi Novemba na kuendelea hadi mwisho wa mwezi.
Kwa hiyo tuanze tafakari hii, sehemu ya kwanza ya Watakatifu. Fundisho kuu tunalopata katika siku hii ya watakatifu wote, ni msisitizo wa maisha yetu kuishia mikononi mwa Mungu aliyetuumba huko mbinguni.

Page 1 of 5