VATICAN CITY, Vatican
Katibu Mkuu wa Vatican, Mwadhama Pietro Kardinali Parolin, ametaka ushiriki wa Marekani na jukumu kubwa kwa Ulaya, katika juhudi za kukomesha mzozo wa Ukraine, akisisitiza kwamba China pia ina neno la kusema kwa ajili ya amani.
Aliyasema hayo hivi karibuni, aliposhiriki katika Hospitali ya Watoto ya Bambino Gesù, akiashiria kumbukumbu ya miaka 40 ya kutambuliwa kwake, kama Taasisi ya Kisayansi ya Kulazwa Hospitalini na Matibabu.
Akizungumzia mkutano na Waziri Mkuu wa Hungaria, Viktor Orbán, aliuelezea kama majadiliano mazuri, na kwamba wanajaribu kuleta misimamo yao karibu zaidi.