Tabora
Na Munir Shemweta
Zoezi la uthamini wa maeneo, yatakayopitiwa na ujenzi wa Mradi wa Reli ya Kisasa (Standard Gage Railway-SGR), kipande cha sita kutoka Tabora hadi Kigoma, linaendelea kwa kasi katika Wilaya sita za mikoa hiyo.
Wilaya hizo ni Tabora Mjini, Uyui, Urambo, Kaliua, Uvinza pamoja na Wilaya ya Kigoma.
Timu kutoka Ofisi ya Mthamini Mkuu wa Serikali, ikiongozwa na Mthamini Kiongozi FRV James Mark Mwanakatwe, ipo mkoani Kigoma, ikiendelea na kazi ya uhamasishaji pamoja na ukusanyaji taarifa za mali uwandani, kwa wananchi ambao maeneo yao yanaguswa na mradi huo.