Mbeya
Na Mwandishi wetu
Maaskofu wa Majimbo mbalimbali ya Kanisa Katoliki nchini, wameadhimisha Misa Takatifu za kuwaombea watu waliouawa na kujeruhiwa, katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29 mwaka huu, huku wakitoa kauli tofauti tofauti na kukemea, kuhusu hali ya uvunjifu wa amani iliyotokea wakati wa uchaguzi huo.