Print this page

Kukauka Mto Ruaha Mkuu pengo kwa hifadhi, uchumi

Dar es Salaam

Na Dk. Felician B. Kilahama

Mapokeo ya kihistoria tangu miaka ya 1880, yanathibitisha kwamba baadhi ya mataifa barani Ulaya mathalani, Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Ubelgiji na Hispania, yaliweza kufika barani Afrika.
Hivyo, 1884 kukafanyika kikao maalumu jijini Berlin-Ujerumani, kwa lengo mahususi kugawana maeneo kuitawala Afrika.
Kwa upande wa Afrika-Mashariki, Wajerumani wakatawala “Tanganyika” na wakaweza kufika maeneo ya Iringa, ambako Hifadhi-Ruaha inapatikana. Wakiwa huko waliona sehemu imesheheni rasilimali nyingi za wanyamapori, na kuifananisha na “Bustani ya Edeni”.
Kiuhalisia Ruaha kuna urithi wa aina yake, mathalani milima na mabonde pamoja na rasilimali-misitu aina ya miombo, misitu inayostawi kandokando ya mito, na Mto Ruaha-Mkuu. Mto huu ni msaada mkubwa aina yake, ikiwemo wanyamapori wanaoishi kwenye hifadhi ya Ruaha.

Rate this item
(0 votes)
Japhet

Latest from Japhet