Na Mwandishi Wetu
Katika makala haya kuhusu Ubatizo wa Bwana, Mwadhama Protace Kardinali Rugambwa katika mahubiri yake, ametumia fursa hii kufafanua alama muhimu, zilizojionesha wakati Kristo Yesu alipobatizwa mtoni Yordani.
Anasema kwamba alama ya kwanza ni Maji: Alama ya kifo na uhai; Mbingu zikamfunukia, Roho Mtakatifu akashuka juu yake kama hua; Alama ya pili ni kufunguka kwa mbingu; Alama ya mabadiliko ya ndani ya mwanadamu, mbele ya Mwenyezi Mungu; Alama ya tatu ni Roho Mtakatifu aliyemshukia Kristo Yesu na sauti ya Baba wa milele ikasikika: Huyu ni mwanangu, mpendwa wangu.
Ubatizo ni sakramenti inayotuingiza katika Ukristo, ni sakramenti inayotuondolea dhambi ya asili na adhabu zake zote. Ni kwa njia ya Ubatizo tunazaliwa upya kwa maji na Roho Mtakatifu, na hivyo tunakuwa ni watoto wa Mungu na wa Kanisa.