Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha
Burudani

Burudani (16)

Dar es Salaam

Na Arone Mpanduka

Bendi ya Extra Musica ambayo ilitamba sana zamani, ilianzishwa mwaka 1993 jijini Brazzaville, Jamhuri ya Congo, ikiasisiwa na wanamuziki akina Ibabi Okambi Rogatien ‘Roga Roga’, ambaye ni mahiri kwa kulicharaza gitaa la solo. Aidha, Roga Roga ndiye kiongozi wa kundi hilo hadi sasa.
Muasisi mwingine ni Espe Bass, ambaye ni muungurumishaji wa gitaa la besi. Mwaka 1995, wanamuziki wa bendi hiyo waliachia albamu yao ya kwanza ya Nouveaux Missiles, iliyowatambulisha vyema kwenye ulimwengu wa muziki.
Albamu hiyo ilipambwa na nyimbo nyingi kali, hususan ule Fred Nelson. Wanamuziki walioshiriki kwenye albamu hiyo, mbali na Roga Roga na Espe Bass, ni pamoja na Guy Guy Fall, Quentin Moyascko, Oxygen Mbon Slyvain, Dou Dou Copa ‘Elenga Laka Bienvenu’, Dominique, Christian na Herman Nagasaki, ambao wote ni waimbaji, pamoja na kunengua.
Wanamuziki wengine walikuwa akina Killa Mbongo aliyekuwa ‘rapa’, Durell Loemba, ambaye ni mcharazaji wa gitaa la rhythm. Kwa upande wa uchanganyaji ‘drums’, yupo Ngolali G’Ramatoulaye na Christian Kingstall aliyekuwa anabofya kinanda.
Wanamziki wa bendi hii ya Extra Musica walijizolea sifa lukuki, wakapendwa na wapenzi wengi kwa jinsi walivyo wajuzi katika kulishambulia jukwaa wakinengua katika maonesho yao yote, ikiwahusisha wanamuziki wenyewe kunengua, tofauti na bendi nyingine ambazo hutumia wanenguaji wa kike.
Ndiyo sababu wao walipenda kujiita ni La Difference, yaani, ni wa tofauti.
Kwenye albamu hiyo ya kwanza, kulikuwa na wanamuziki wengine ambao hawakupata nafasi ya kurekodi, wakiwemo akina Pinochet Thierry, Regis Touba, Cyrille Molanga na Arnaud Luguna.
Albamu hiyo ya Nouvoeaux Missiles, ilisababisha wanamuziki wengine nje ya bendi yao kuvutiwa nayo, mmojawapo alikuwa Samba Brice Abillissi, aliyeamua kujiunga nao.
Albamu ya pili ya Confirmation ya mwaka 1996, ilipelekea kundi hilo kuzidi kutikisa vilivyo, hadi wakapata mialiko mingi barani Afrika na Ulaya.
Inaelezwa kuwa albamu hiyo ya Confirmation iliuza nakala nyingi mno kuzidi ile ya mwanzo.
Lakini mafanikio hayo yalisababisha kuzuka kwa mgogoro mkubwa wa kimasilahi, hali iliyofanya baadhi ya wanamuziki wake wakiwamo akina Christian na Guy Guy Fall, kujiondoa kundini, japokuwa kuondoka kwa wanamuziki hao, Extra Musica iliendelea kuwa imara.
Ilipotoka albamu ya tatu ya Ouragan mwaka 1997, wanamuziki Herman Nagassaki na Samba Brice Abilliss, waliziba vilivyo mapengo ya Guy Guy Fall na Christian.
Mgogoro wa chini kwa chini ulikuwa ukifukuta miongoni mwa wanamuziki wa bendi hiyo, na uongozi. Baadhi ya wanamuziki walishindwa kuvumilia, wakaihama bendi hiyo. Wanamuziki hao walikuwa ni Arnaud Laguna, Quentin Mayascko, Durell Loemba, Cyrille Malonga, Regis Touba na Pinochet Thierry.
Wakaenda kuunda kundi lao jingine walilolipa jina la Z.I. International, chini ya uongozi wa Cyrille Malonga, Regis Touba, Pinochet Thierry na Durrell Loemba.
Baada ya bendi ya Extra Musica kukimbiwa na wanamuziki hao, walikaa chini na kuamua kuwatafuta wanamuziki wengine vijana wenye vipaji vikubwa.
Walifanikiwa kuwapata vijana hao akina Gildas Pozzi, na Emery Mboma. Wakati huo huo, Sonor alichukua nafasi ya ucharazaji wa gitaa la rhythm lilokuwa likishikwa na Durell Loemba.
Mara baada ya kuwaingiza vijana hao kundini, mwaka 1998 waliachia albam yao ya nne ya Extra Major. Albamu hiyo ilivunja rekodi ya mauzo ya albamu zote za awali na kuwaletea tuzo nyingi Barani Afrika, ikiwemo ya Kora kwa kuteuliwa kuwa bendi bora ya muziki katika Bara la Afrika.
Mwaka uliofuatia, waliachia albamu nyingine tano zilizokuwa kali mno.
Kati ya albamu hizo ile ya Shalai ilisababisha kuwapata wanamuziki wengine wakali, akina Papy Batin Maboulango na Boudouin Massipi.
Rapa wao wa kutumainiwa Killa Mbango, alijitoa kundini akaachana na muziki. Lakini baadaye alirejea kundini. Extra Musica, japo ilichukua kipindi kirefu kutoa albamu ya sita ya Trop C’Est Trop katika mwaka 2001.
Rapa mwingine alijulikana kwa jina la Arafat, nae alijiunga na bendi hiyo, akichukua nafasi iliyoachwa wazi kwa mara nyingine tena, na Killa Mbongo.
Baada ya kutoka na albamu hiyo, waliamua kubadilisha kidogo majina ya bendi yao ikaitwa Extra Musica Zagul.
Mara baada ya kutoa albamu ya saba ya Obligatoire mwaka 2004, mwimbaji wao Dou Dou Copa naye akajiondoa kundini, akafuatiwa na Oxygene mwaka 2005.Kuodoka kwa wanamuziki hao hakukuathiri Extra Musica Zagul, kwani waliachia albamu ya nane ya La Main Noire mwaka 2006, na nyingine ya tisa ya Sorcellirie ‘Kindoki’ katika mwaka 2011.
Licha ya hekaheka nyingi, bendi ya Extra Musica ilisimama tena na kwa sasa muasisi Roga Roga bado anakomaa na kundi la Extra Musica Original, huku wimbo wa Bokoko uliotoka mwaka 2021, ukiendelea kuwa maarufu.

Na Arone Mpanduka

Chimbuko la bendi ya Maquis du Zaire kwa nchi ya Tanzania lilianzia mwaka 1973, wakati Franco Luambo Luanzo Makiadi akiwa na bendi yake ya T.P. OK. Jazz alikuja hapa nchini na akafanya onyesho kamambe katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam(sasa uwanja wa Uhuru).
Mwaka mmoja baadae wa 1972, bendi ya Maquis du Zaire, nayo ikaingia kwa mbwembwe na kuweka makazi yake ya kudumu katika jiji la Dar es Salaam.
Bendi hiyo Maquis du Zaire iliyotokea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ikafia humu nchini miaka ya 1990.
Ilikuwa kivutio kikubwa kwa Watanzania na kuwapa hekaheka wanamuziki wa Tanzania katika miaka hiyo.
Kwa nchini Congo, bendi hiyo ilianza mwaka 1960, vijana wa wakati huo katika mji wa Kamina huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), waliungana na kuunda bendi yao, wakaiita Super Theo.
Bendi hiyo ilikuwa ikitoa burudani tosha kwa wapenzi wa muziki wa mji huo wa Kamina na vitongoji vinavyouzunguka mji huo. Baadae wakaibadilisha majina na bendi ikawa Super Gabby. Lakini uongozi wa Super Gabby ulitaka kuleta mageuzi katika muziki mwaka 1972, walipobadilisha majina rasmi na kuwa Maquis du Zaire.
Mwaka huo huo bendi hiyo iliingia hapa Tanzania wakipitia nchini Uganda.
Walipofika katika jiji la Dar es Salaam, walipata mkataba wa kupiga muziki katika ukumbi wa Mikumi Tours, uliokuwa maeneo la Tazara Buguruni, jijini Dar es Salaam.
Baada ya kumaliza mkataba wao, waliondoka wakaenda kupiga muziki katika Klabu ya Hunters kwa kipindi kifupi.
Kisha viongozi wa bendi hiyo wakafanya mazungumzo na mfanyabiashara Hugo Kisima, aliyekuwa akimiliki ukumbi wa Safari Resort, maeneo ya Kimara, jijini Dar es Salaam. Wakaanza kupiga muziki kwa mkataba na mfanyabiashara huyo.
Februari 1977 viongozi wa bendi hiyo ya Maquis du Zaire, waliamua kukiongezea nguvu kikosi chao. Hivyo walimtuma Tchibangu Katayi ‘Mzee Paul’ aliyekuwa mwanamuziki wa bendi ya Maquis du Zaire.
Pia alikuwa mmoja kati ya viongozi wa bendi hiyo.Mzee Paul aliwachukua baadhi ya wanamuziki ili kuja nao Tanzania kuongeza nguvu katika bendi ya Maquis du Zaire.
‘Mzee Paul’ alibahatika kuwachukua wanamuziki akina Kikumbi Mwanza Mpango, au ‘King Kiki’, mtunzi na mwimbaji, Kanku Kelly kwa upande wa tarumbeta., Ilunga Banza ‘Mchafu’, aliyekuwa akiungurumisha gitaa la besi, Mutombo Sozy aliyekuwa akizicharanga ‘drums’, na mnenguaji Ngalula Tshiandanda.
Wakati huo Maquis du Zaire walikuwa wakicheza muziki wakitumia mtindo wa ‘Chakula Kapombe’, ambao kwa Watanzania ulikuwa mpya, na ukapendwa mno na mashabiki.
Kufika kwa wanamuziki hao, kulileta changamoto kubwa katika muziki. Tungo nzuri za Kikumbi Mwanza Mpango ‘King Kiki’, zilikuwa chachu masikioni mwa wapenzi wa muziki wa dansi. Kiki pia yaelezwa kuwa ndiye aliyeleta Mapinduzi makubwa ya muziki hapa nchini Tanzania.
Maquis du Zaire wakaazisha mtindo mwingine wa ‘Kamanyola’, uliowapagaisha wapenzi na wadau toka pembe zote za jiji la Dar es Salaam.
Mwishoni mwa 1977, Marquis du Zaire walimaliza mkataba kwa Hugo Kisima, wakaondoka.Bahati nyingine ikawadondokea tena baada ya kuingia mkataba mwingine wa kupiga muziki kwa mzee Makao, aliyekuwa akimiliki ukumbi wa Savannah, maeneo ya Ubungo.Wakiwa Savannah, walianzisha mitindo ya ‘Sanifu’, na ‘Ogelea piga mbizi’.
Lakini ukumbi huo ukabadilishwa jina ukaitwa White House. Ikumbukwe kwamba Maquis pia ilikuwa ikipiga kwenye ukumbi wa Mpakani, maeneo ya Mwenge.Mwishoni mwa mwaka 1978, Maquis du Zaire  waliamua kuimarisha tena kikosi chao kwa kuwaleta wanamuziki wengine wapya kutoka DRC.Iliwaleta akina Kabeya Badu, Kalala Mbwebwe, Ngoyi Mubenga na Khatibu Iteyi Iteyi.
Bendi hiyo ilikuwa ikiongozwa na wanahisa akina Chinyama Chiyaza ‘Chichi’, Chibangu Katayi ‘Mzee Paul’, Chimbwiza Mbangu Nguza au ‘Nguza Vicking’, Mutombo Lufungula ‘Audax’ na Mbuya Makonga ‘Adios’.
Chini ya uongozi huo, katika miaka ya 1980 mafanikio makubwa yalionekana, mojawapo ni lile la kuanzisha Kampuni iliyofahamika kama Orchestra Maquis Company (OMACO).
Kampuni hiyo iliweza kumiliki shamba la matunda, wakalima kwa kutumia trekta zao maeneo ya Mbezi nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam. Mazao yao walikuwa wakiyapeleka na kuuza katika Soko Kuu la Kariakoo jijini Dar es Salaam.OMACO pia ilimiliki mradi mwingine wa viwanja tisa na nyumba kadhaa, maeneo ya Sinza, jijini Dar es Salaam.
Kwa wakati huo, watu wengi hawakuwa na haja ya kuchukua teksi kurudi nyumbani, kwani muziki wa Maquis du Zaire ulikuwa unarindima hadi alfajiri. Muda ambao mabasi ya UDA ya Ikarus yalikuwa yameanza kazi. Wakati huo hazikuwepo ‘Dala dala’, Bajaji wala Pikipiki kwa maana ya Bodaboda.
Hata hivyo, baadae bendi hiyo ilianza kufa taratibu kufuatia baadhi ya wanamuziki kuondoka kwenda kutafuta maisha sehemu nyingine, na wengine kusahindwa kufanya kazi hiyo kutokana na umri kuwa mkubwa, na magonjwa ya hapa na pale.
Mwanzoni mwa miaka ya 1990, bendi ilipotea kabisa na kuacha historia ya kipekee.
Baadhi ya nyimbo za Marquis du Zaire zilizovuma kwa uzuri na utamu wake ni ‘Ni Wewe Pekee; Makumbele; Kalubandika; na Promotion’.
This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.

Page 2 of 2