Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

DAR ES SALAAM

Na Nicholas Kilowoko

Kocha wa vijana wa klabu ya soka ya Simba, John Bocco, ameelezea mikakati yake mipya ya kuisaidia timu yao kubwa, kupata vijana wazawa wenye vipaji na watakaolisaidia Taifa pia.
Kwa muda mrefu nyota huyo wa zamani, ambaye alifanya makubwa ndani ya klabu ya Simba, Azam FC, na JKT Tanzania, alikuwa yupo kimya mara baada ya kumaliza kazi yake ya uchezaji.

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Mkuu wa Kitengo cha Habari cha klabu ya soka ya Azam FC, Thabit Zacharia maarufu kama Zaka Zakazi, amesema kuwa kitakwimu winga wa Taifa Stars Simon Msuva, bado ataendelea kuwa juu katika ufungaji wa mabao mengi katika kikosi hicho, kuliko mchezaji mwingine yoyote.
Akitoa ufafanuzi kuhusiana na ubishani unaoendelea, wa kumlinganisha Msuva na mchezaji wa zamani wa Taifa Stars Mrisho Ngassa, Zaka alisema kwamba nyota hao wanalinganishwa kimakosa, kwa sababu Msuva ana mabao 21 aliyoifungia Taifa Stars pekee, huku Ngassa mabao yake yakichanganywa na aliyoifungia Kilimanjaro Stars, ambayo ni ya Tanzania Bara pekee.

London, Uingereza
Meneja wa Arsenal Mikel Arteta, amekiri kuwa watakuwa wakiangalia kwa makini usajili unaowezekana, wakati wa dirisha la uhamisho la Januari.
The Gunners walitumia takribani pauni milioni 250 msimu huu wa joto, na kuleta wachezaji wapya nane, huku wakitafuta kuongeza ubora katika kikosi chao, ili kukabiliana na orodha ya mechi zilizojaa, na kushindania mataji katika mashindano mengi.
Msimu uliopita kampeni ya Arsenal iliharibiwa na majeraha, kwani walikuwa bila mlinzi Gabriel Magalhaes, kwa sehemu ya mwisho ya msimu na walicheza na kiungo Mikel Merino, kama mshambuliaji wa muda, walipomaliza wa pili katika Ligi Kuu kwa msimu wa tatu mfululizo, na walitolewa katika nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa na Paris St-Germain.
Msimu huu The Gunners pia wamekuwa wakisumbuliwa na majeraha, mara baada ya kumpoteza Kai Havertz tangu siku ya ufunguzi, huku nahodha Martin Odegaard na Bukayo Saka, Gabriel Martinelli, Noni Madueke na Max Dowman wakiwa wamekosa nafasi.
Sasa baada ya majeraha kuwaathiri zaidi wachezaji washambuliaji, ni safu ya nyuma ya Arsenal inayoteseka, Arteta alilazimika kumchezesha Declan Rice, katika nafasi isiyojulikana ya beki wa kulia dhidi ya Brighton siku ya Jumamosi, kwa sababu Jurrien Timber alikuwa majeruhi, na Riccardo Calafiori alipata tatizo wakati wa mazoezi ya kupasha misuli.

Melboune, Australian
Uwanja wa Kriketi wa huko mjini Melbourne umekadiriwa kuwa hauridhishi, Baraza la Kriketi la Kimataifa (ICC) limethibitisha.
Uamuzi huo unamaanisha kuwa, Uwanja wa Kriketi wa Melbourne unapata pointi moja ya upungufu. Ikiwa uwanja unapata pointi sita za upungufu katika kipindi cha miaka mitano, unasimamishwa kuandaa kriketi ya kimataifa kwa miezi 12.
Ni mara ya kwanza uwanja nchini Australia, kuonekana kuwa chini ya kiwango, tangu ICC ibadilishe mfumo wake miaka miwili iliyopita.
Wiketi thelathini na sita zilianguka katika vipindi sita katika mechi ya Boxing Day, huku harakati nyingi za kushona zikitolewa kwa wapiga mpira wa kasi.
“Kwa wiketi 20 zikianguka siku ya kwanza, 16 siku ya pili na hakuna mpigaji hata mmoja aliyefikia nusu karne, uwanja ulikuwa hauridhishi kulingana na miongozo, na uwanja unapata pointi moja ya upungufu,” alisema mwamuzi wa mechi Jeff Crowe.

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Mchezo wa skwashi ulianzishwa karne ya 19 nchini Uingereza. Ulianza kama mabadiliko ya mchezo wa racquetball, na kuendelezwa katika shule za wasichana na wavulana. 
Mchezo huu ulienea haraka katika nchi za Uingereza, kisha ulienea duniani kote, hasa katika nchi zilizoathiriwa na Wazungu kama Canada, Marekani, Australia, na baadhi ya nchi za Afrika.

DAR ES SALAAM

Na Remigius Mmavele

Rigobert Bamundele Ifoli, maarufu kwa jina  Rigo Star, alizaliwa Agosti 28,1955 jijini Kinshasa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).Rigo Star ni mpiga gita hodari aliyetikiza duniani kwa kupiga chombo hicho, alianza kuonyesha uwezo wake akiwa na umri mdogo ambapo alikuwa mmoja wa wapiga gitaa wenye ushawishi mkubwa nchini mwake.

Katika safu hii ya Chimba Chimba Historia ya Kanisa wiki iliyopita, tuliendelea kuwaletea historia ya mitaguso mikuu, kwa kuendelea na Mtaguso Mkuu wa Kostantinopole. Leo tunawaletea historia ya kuasi kwa Kanisa la Wakopti Misri, na historia ya Mababa wa Kanisa wa Magharibi. Sasa endelea…

Bahati mbaya, Wakristo wa Misri ambao kabla walikuwa kila mara wanashinda, na hivyo wakajiona kama watetezi imara wa imani, mara hii waliposhindwa hawakufurahi. Walishinda wakati wa Arius na walishinda wakati wa Nestorius, lakini sasa kwa kusisitiza mno umoja na umungu wa Kristo walishindwa. 

Hawakupokea kushindwa, hivyo Kanisa zima likaendelea na uzushi huo ulioitwa ‘Monophysitism’, maana yake Yesu  ni Mungu na utu wake umekandamizwa. 

Bagamoyo

Na Laura Mwakalunde

Askofu wa Jimbo la Bagamoyo, Mhashamu Stephano Musomba, amewataka Waamini kutokuwa na Roho dhaifu, za kushindwa kuvumilia shida na matatizo.
Askofu Musomba alisema hayo hivi karibuni, wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika ya Tatu ya Furaha ya Majilio, iliyofanyika katika Parokia ya Bikira Maria wa Mlima Karmeli-Bunju, jimboni humo.

Mgeta

Na Angela Kibwana

Zaidi ya watoto Wamisionari 300 wa Shirika la Kipapa, Dekania ya Mgeta Jimboni Morogoro, wameshiriki Kongamano la kufunga mwaka, katika dekania hiyo.
Kongamano hilo limefanyika katika Parokia ya Bikira Maria wa Mlima Karmeli-Mgeta, Morogoro, likihusisha watoto kutoka Parokia sita zinazounda Dekania hiyo, kama njia mojawapo ya kuwakuza watoto kiimani na kimaadili, kupitia mafundisho ya semina na michezo mbalimbali.

Dar es Salaam

Na Laura Mwakalunde

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi, amewataka Waamini kutambua kwamba, Karamu ya Sakramenti Takatifu haikuja ili kushibisha tumbo.
Askofu Ruwa’ichi alisema hayo hivi karibuni, wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya kuzindua Mnara wa Kanisa, iliyofanyika Parokia ya Mwenyeheri Anuarite-Makuburi, jimboni humo.

Page 1 of 59